Mitazamo ya Kiyahudi juu ya Yesu

Mitazamo ya Kiyahudi juu ya Yesu ni ya aina mbalimbali, lakini yote haimkubali, la sivyo ingewabidi wahusika wamuamini na kubatizwa badala ya kuendelea na dini yao ambayo viongozi wake walimhukumu ni kafiri anayestahili kuuawa.

Johann von Armssheim (1483) alivyochora mabishano kati ya wataalamu Wakristo na Wayahudi.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Kwa kawaida Wayahudi wanamuona Yesu kama mmojawapo kati ya wengi waliojinadi kuwa Masiya katika nyakati mbalimbali za historia ya taifa lao.[1]

Yesu anatazamwa kama yule aliyefaulu zaidi kukubalika, na kwa sababu hiyo, kuleta madhara makubwa kuliko wote.[2]

Uyahudi haujawahi kumkubali rasmi Masiya yeyote kuwa ametimiza utabiri wa manabii. Zaidi ya hayo, unaona ibada ya Wakristo kwa Yesu kuwa kinyume cha imani katika Mungu mmoja tu.[3]

Katika Karne za Kati, Judah Halevi na Maimonide walimuona Yesu (kama vile Muhammad) kama mtu muhimu katika kuandaa mataifa yote kwa ujio wa Masiya atakayeyafanya yamuabudu Mungu pekee.

Siku hizi kuna wataalamu Wayahudi wanaosema Yesu alikuwa jirani na dini yao kuliko Injili zinavyoonyesha. Mtazamo huo ulianzishwa katika karne ya 18 na Jacob Emden na Moses Mendelssohn.

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mitazamo ya Kiyahudi juu ya Yesu kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Viungo vya nje hariri

  1. Jesus of Nazareth
  2. Maimonides. Mishneh Torah, Sefer Shofetim, Melachim uMilchamot, Chapter 11, Halacha 4. Chabad translation by Eliyahu Touge.
  3. Devarim (Deuteronomy) 6:4