Mjusi-nyungunyungu

Mjusi-nyungunyungu
Mjusi-nyungunyungu wa Lang (Chirindia langi)
Mjusi-nyungunyungu wa Lang (Chirindia langi)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli ya juu: Tetrapoda
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Amphisbaenia (Mijusi-nyungunyungu)
Ngazi za chini

Familia 6:

Mijusi-nyungunyungu ni wanyama watambaachi katika oda Squamata ya ngeli Reptilia. Wanyama hawa hawafikiriwi kuwa mijusi wa kweli, lakini wataalamu wengine wanafikiri kwamba wana nasaba na familia ya mijusi Lacertidae.

Kama jina lao linadokeza, mijusi-nyungunyungu wanafanana na nyungunyungu kwa sababu hawana miguu, ngozi ya takriban spishi zote ni pinki na magamba yanatungamanika katika miviringo. Hata huishi ndani ya udongo kama nyungunyungu. Kwa hivyo hawana masikio ya nje na macho yamo katika vishimo na yamefunika kwa ngozi na gamba. Wanaweza kushufu nuru kwa sababu macho bado yana kornea na lenzi.

Mijusi-nyungunyungu hula wadudu na lava wao na invertebrata wengine kama nyungunyungu.

Spishi za Afrika ya Mashariki hariri