Mtemi Mirambo (1840-1884) alikuwa mtemi wa Wanyamwezi katika magharibi ya Tanzania ya leo.

Mirambo katika miaka ya 1880, kabla ya kifo chake
Historia ya Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
This article is part of a series
Uendo
Historia ya Zanzibar
Afrika Mashariki 1800-1845
Ukoloni
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland
Mkwawa
Vita vya Maji Maji
Vita vikuu vya kwanza Afrika Mashariki
Tanganyika
Mapambano ya uhuru Tanganyika
Uhuru
Uhuru wa Tanganyika
Mapinduzi ya Zanzibar
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Julius Nyerere
Ujamaa
Tamko la Arusha
Vita vya Kagera
Ali Hassan Mwinyi
Benjamin Mkapa
Jakaya Kikwete
John Magufuli
Samia Suluhu Hassan

Tanzania Portal

Jina lake la awali lilikuwa "Mteyla Kasanda", lakini alikuwa maarufu zaidi kama Mirambo (yaani "maiti nyingi"). Alizaliwa kama mwana wa mtemi wa Uyowa, moja kati ya maeneo madogo ya Unyamwezi akarithi utemi kutoka babake mnamo mwaka 1860.

Mirambo alitajirika kama mfanyabiashara ya pembe za ndovu na watumwa kwa njia ya misafara kati ya pwani ya Bahari Hindi na Kongo.

Alitumia sehemu kubwa ya utajiri wake kujenga jeshi la binafsi. Kwa kusudi hilo alinunua bunduki aina ya gobori na kukusanya vijana wengi walioitwa "rugaruga". Rugaruga hao walihofiwa kote. Inasemekana ya kwamba kabla ya mapigano walipewa pombe na bangi kwa kusudi la kuongeza ukatili na kupunguza hofu yao ya kifo.

Kwa kawaida vijana hao walikuwa wanaume walioishi bila ukoo na bila familia kisha kutoroka kwenye hali ya utumwa au kuwa wapagazi wa misafara.[1][2] Mirambo aliwapokea na kuwapa silaha na kwa njia hii alishinda maadui na aliweza kupanua eneo lake hadi kuwa mtemi mkuu wa Wanyamwezi[3][4] kuanzia mwaka 1860 hadi kifo chake mnamo 1884[5].

Alisifiwa na Henry Morton Stanley kama "Napoleon Bonaparte Mwafrika" kutokana na ushujaa wake dhidi ya Waarabu waliomuunga mkono Stanley mwenyewe. Hata hivyo hakufaulu kuteka Tabora kutoka mikononi mwao.

Tanbihi hariri

  1. John Iliffe: A Modern History of Tanganyika. Cambridge University Press, Cambridge 1979, uk. 64
  2. The Cambridge History of Africa, vol. 6
  3. The Nyamwezi aristocracy was appalled when someone who was not royalty took over the religiously ceremonial office of ntemi.
  4. The Cambridge History of Africa, vol. 5
  5. It is possible that he was strangled to death, since an old Nyamwezi custom was to strangle their mtemi when they became unfit to rule.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtemi Mirambo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.