Mundu ni kifaa kinachotumiwa katika kilimo kwa kukata nyasi na mavuno ya nafaka na mazao mengine.

Mundu
Mundu na nyundo katika nembo la Austria

Mundu kama zana ya kilimo inajulikana tangu zama za mawe.

Katika nchi nyingi za dunia haitumiwi tena sana kwa sababu nafasi yake imechukuliwa na mashine lakini pale ambako kazi ya kilimo inatekelezwa kwa mkono ni mahali pake hadi leo.

Umbo la mundu ni kama kisu kirefu kilichopindwa kama kotama ndefu. Upande wa ndani ya bapa ni kali, upande wa nje ahuna ukali.

Umbo la mundu lilitumiwa pia kama silaha kwa aina za pekee za upanga.

Katika nembo la Austria na pia la Umoja wa Kisovyeti wa zamani mundu ni alama ya wakulima ikionyeshwa pamoja na nyundo kama alama ya wafanyakazi.