Mwanajimbo ni neno linalotumiwa hasa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kuhusu mwamini wake ambaye anategemea jimbo katika shughuli zake za kichungaji au za kiroho kwa jumla.

Kwa namna ya pekee linatumika kuhusu padri au shemasi ambaye ameandikishwa na jimbo kama mmojawapo wa viongozi wake wa kudumu, tofauti na mtawa ambaye ameandikishwa rasmi katika shirika lake.

Pengine katika historia ya Kanisa aina hizo mbili za kleri zilishindana sana upande wa wajibu na haki hasa kuhusu uchungaji katika parokia na makanisa mengine.

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.