Mwanasheria Mkuu ni mtaalamu wa sheria mwenye kazi ya kushauri serikali au mahakama katika utekelezaji wa majukumu yake.

Nafasi hii inapatikana katika nchi mbalimbali hasa kama zinazothiriwa na haki ya Uingereza yaani katika koloni zake za zamani.

Anaweza kuchaguliwa na bunge, na rais au kamati za pekee.

Tanzania hariri

Kufuatana na kifungu 79 cha katiba ya Tanzania mwanasheria mkuu anashiriki katika mikutano ya baraza la mawaziri, kazi yake ni kuwa mshauri mkuu wa serikali katika masuala ya kisheria, kuwakilisha na kutetea serikali mahakamani au hata kutoa shauri la kisheria kwa mahakimu[1].

Mwanasheria mkuu wa Tanzania anateuliwa na rais tu. Anaweza kuwa mbunge kutokana na wahifadhi wake na atashika madaraka yake mpaka uteuzi wake utakapofutwa na rais au mara tu kabla ya rais mteule kushika madaraka.

Wafuatao waliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa Tanzania:

Kilangi alirudishwa katika nafasi hiyo tarehe 5 Novemba 2020 akithibitishwa katika cheo chake na rais John Pombe Magufuli[2].

Marejeo hariri

  1. The Constitution of the United Republic of Tanzania of 1977, tovuti ya WIPO (World Intellectual Property Organization ), iliangaliwa Novemba 2020
  2. NEW ATTORNEY GENERAL PROMISES DILIGENCE, blogu ya http://ardenkitomaritz.blogspot.com ya tar. 7-02-2018