Mwangaza halisi (kwa Kiingereza absolute magnitude) ni kipimo cha ukali wa nuru ya nyota au magimba mengine ya anga jinsi itakavyoonekana kwa mtazamaji aliye kwa umbali sanifu wa miakanuru 32.6 au parsek 10.

Mwangaza halisi ni tofauti na mwangaza unaoonekana jinsi tunavyoona nyota kutoka Dunia. Maana mwangaza tunaoona unategemea na ukubwa wa nyota, umbali wake na mambo mengine. Nyota ndogo na hafifu iliyo karibu nasi katika anga-nje itaonekana angavu kuliko nyota kubwa iliyo mbali. Hii ni sawa na kuangalia taa iliyo karibu au mbali.

Kipimo hiki kwa kutumia umbali sanifu kinawaruhusu wanaastronomia kulinganisha uang'avu wa magimba.

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mwangaza halisi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.