Panfilo na wenzake

Panfilo na wenzake (walifia dini Kaisarea Baharini, leo nchini Israeli, 16 Februari 309) ni kundi la Wakristo 12 waliouawa huko Kaisarea ya Palestina kwa ajili ya imani yao katika dhuluma ya kaisari Maximian.

Wa kwanza kuuawa walikuwa Wakristo 5 wa Misri: Elia, Yeremia, Isaya, Samweli na Danieli ambao waliteswa na hatimaye kuuawa kwa upanga.

Baada yao waliuawa padri Panfilo (mzaliwa wa Beirut, leo nchini Lebanoni), shemasi Valens wa Yerusalemu, Paulo wa Iamnia, Porfiri, Seleuko wa Kapadokia, Teodulo na hatimaye Juliani wa Kapadokia aliyechomwa moto taratibutaratibu.

Sifa yao imedumishwa na maandishi ya Eusebi wa Kaisarea, aliyekuwa mwanafunzi wa Panfilo na ameshuhudia pia utaalamu wake kuhusu Biblia[1].

Panfilo aliandika vitabu vitatu vya kumtetea Origen, lakini kimetufikia cha kwanza tu.

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe ya kifo chao[2] au tarehe 1 Juni[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.