Panteno (kwa Kigiriki: Πάνταινος; alifariki 200 hivi[1]) alikuwa mmoja wa wanateolojia wa kwanza katika historia ya Kanisa, mwenye hekima kubwa na ari ya kitume [2].

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi wa Mashariki na Wakatoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa nao tarehe 22 Juni na 7 Julai[3][4].

Maisha hariri

 
Ramani ya Barabara ya hariri ikionyesha njia za zamani kati ya mabara.

Mzaliwa wa kisiwa cha Sisilia (Italia) Panteno alikuwa mwanafalsafa mwenye kufundisha mjini Aleksandria.[5] Baada ya kuongokea Ukristo, alijitahidi kulinganisha imani yake mpya na falsafa ya Ugiriki wa Kale.[6][7] Hata hivyo hakuna maandishi yake yoyote yaliyobaki hadi leo.[8]

Aliongoza Chuo cha Kikristo cha Aleksandria (Misri) kuanzia mwaka 180 hivi. Ndicho chuo cha kwanza cha katekesi, nacho kiliathiri sana teolojia ya baadaye, hasa juu ya Biblia, Utatu, Kristo. Kilipoanzishwa kusudi lake lilikuwa kuwaelimisha Wapagani waliotafuta habari za imani mpya ya Kikristo kabla ya ubatizo. Chuo cha Aleksandria kikaendelea haraka kuwa kitovu cha elimu ya Kikristo na majadiliano kati ya imani ya Kikristo na falsafa ya Kigiriki iliyostawi sana Aleksandria, mji mkuu wa Misri wakati huo.

Kadiri ya Jeromu chuo cha Aleksandria ilianzishwa na Mwinjili Marko. Baadaye anatajwa Athenagora wa Athene (176), lakini kwa hakika zaidi Panteno, aliyeacha uongozi kwa mwanafunzi wake bora, Klementi wa Aleksandria mwaka 190.[9] Huyo alifuatwa na Origene akiwa na umri wa miaka 18 tu, na wataalamu wengine wanaoheshimiwa kama watakatifu katika Kanisa la Kiorthodoksi na Kanisa Katoliki kama Gregori Mtendamiujiza, Heraklas, Dionisi wa Aleksandria na Didimo Kipofu.

Eusebi wa Kaisarea anasimulia kuwa Panteno, kutokana na upendo wake kwa Neno la Mungu, alikwenda kama mmisionari[10] kuinjilisha watu wa mashariki hadi India.[11][12][13][14][15][16].

Hatimaye alirudi Aleksandria, alipofariki dunia kwa amani wakati wa kaisari Caracalla[17].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. "As he was succeeded by Clement who left Alexandria about 203, the probable date of his death would be about 200. " (Catholic Encyclopedia)
  2. https://dacb.org/stories/egypt/pantaenus/
  3. Martyrologium Romanum
  4. http://catholicsaints.info/saint-pantaenus-of-alexandria/
  5. Alban Butler; Paul Burns. Butler's Lives of the Saints, Volume 7. A&C Black. uk. 48. 
  6. Cf. Article "Clement of Alexandria" in the St. Thomas Christian Encyclopaedia of India, Ed. George Menachery, Vol. II, 1973, p.201
  7. Clement, Stromata, 1.1.
  8. Although Lightfoot (Apost. Fathers, 488), and Batiffol (L'église naissante, 3rd ed., 213ff) attribute the concluding passages of the Epistle to Diognetius to Pantaeus; see "Pantaenus" in The Westminster Dictionary of Christian History, ed. Jerald Brauer.
  9. Cross, F.L.; Livingstone, E.A., eds. (1974). "Clement of Alexandria, St.". The Oxford Dictionary of the Christian Church (2 ed.). Oxford: Oxford University Press.
  10. Cf.Article "Christian Influences on Hinduism before the European Period" by P. Thomas in the St. Thomas Christian Encyclopaedia of India, Vol.II, 1973, p. 177 et. sq.
  11. Church History by Eusebius. Book V Chapter 10. Pantaenus the Philosopher.
  12. Article by S. S. Koder, "History of the Jews in Kerala", in the St. Thomas Christian Encyclopaedia of India, Vol. II, 1973, pp.183 ff.
  13. The Encyclopedia of Christianity, Volume 5 by Erwin Fahlbusch. Wm. B. Eerdmans Publishing - 2008. p. 285. ISBN 978-0-8028-2417-2.
  14. The Jews of India: A Story of Three Communities by Orpa Slapak. The Israel Museum, Jerusalem. 2003. p. 27. ISBN 965-278-179-7.
  15. Cyclopaedia of India and of Eastern and Southern Asia. Ed. by Edward Balfour (1871), Second Edition. Volume 2. p. 584.
  16. Jeromu, De viris illustribus 36
  17. https://www.santiebeati.it/dettaglio/61010

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.