Papa Marcello I alikuwa Papa kuanzia mwaka 306 hadi kifo chake tarehe 16 Januari 309[1]. Alitokea Roma, Italia.

Papa Marcello I.

Alimfuata Papa Marcellinus miaka miwili hivi baada ya huyo kufa wakati wa dhuluma ya Kaisari Diokletiano dhidi ya Wakristo[2] .

Katika kurudisha taratibu za Kanisa, alipanga malipizi makali kwa waumini wengi waliowahi kuasi. Kadiri ya Papa Damaso I, Marseli alikuwa mchungaji bora, aliyepingwa vikali na Wakristo waasi waliokataa kufanya toba aliyokuwa ameiagiza[2], akasingiziwa akafungwa na Kaisari Maxentius na kufariki mapema uhamishoni, akifuatwa madarakani na Papa Eusebius[3].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 16 Januari[4].

Tazama pia hariri

Maandishi yake hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. 2.0 2.1   One or more of the preceding sentences incorporates text from a publication now in the public domainHerbermann, Charles, ed. (1913). "Pope St. Marcellus I". Catholic Encyclopedia. Robert Appleton Company.
  3. Kigezo:EB1911
  4. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Marcello I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.