Papa Sixtus III alikuwa Papa kuanzia tarehe 31 Julai 432 hadi kifo chake tarehe 19 Agosti 440[1]. Alitokea Roma, Italia.

Mtakatifu Sisto III.

Alimfuata Papa Selestini I akafuatwa na Papa Leo I.

Chini yake makanisa mbalimbali yalijengwa mjini Roma, hasa basilika la Bikira Maria lililowekwa wakfu kwa Mama wa Mungu kadiri ya sifa aliyopewa na Mtaguso wa Efeso (431). Pia alijitahidi kupatanisha maaskofu wa Mashariki (Aleksandria na Antiokia) na kutetea mamlaka ya Kanisa la Roma juu ya Iliriko.

Rafiki wa Agostino wa Hippo[2], tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, hasa tarehe ya kifo chake[3].

Tazama pia hariri

Maandishi yake hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. "St. Sixtus III, Pope", Catholic News Agency, March 28, 2017. Jalada kutoka ya awali juu ya 2017-09-16. Iliwekwa mnamo 2022-04-10.
  3. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
  Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Sixtus III kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.