Papa Stefano I alikuwa Papa kuanzia tarehe 12 Machi 254 hadi kifodini chake tarehe 2 Agosti 257[1][2]. Alitokea Roma, Italia, ingawa aliweza kuwa na asili ya Ugiriki.

Alimfuata Papa Lucius I akafuatwa na Papa Sisto II.

Alifundisha kwamba waliobatizwa na madhehebu yaliyojitenga na Kanisa Katoliki wameungana na Kristo moja kwa moja, hivyo hawahitaji wala hawatakiwi kubatizwa tena[3], tofauti na walivyodai baadhi ya maaskofu, hasa wa Afrika Kaskazini. Baadaye msimamo wake ulienea kote katika Kanisa la Kilatini.

Inasimuliwa kwamba aliuawa na maaskari wa Kaisari Valerian wakati wa Misa[4] .

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, pengine mfiadini.

Sikukuu yake ni tarehe 2 Agosti [5].

Tazama pia hariri

Maandishi yake hariri

Marejeo hariri

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. Mann, Horace (1912). "Pope St. Stephen I" in The Catholic Encyclopedia. Vol. 14. New York: Robert Appleton Company.
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/89023
  4. The golden legend: readings on the saints By Jacobus de Voragine, William Granger Ryan
  5. "Martyrologium Romanum" (Libreria Editrice Vaticana, 2001 ISBN 88-209-7210-7)

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Stefano I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.