Peramiho ni kata ya Wilaya ya Songea Vijijini katika Mkoa wa Ruvuma, Tanzania, yenye postikodi namba 57213.

Peramiho
Peramiho is located in Tanzania
Peramiho
Peramiho

Mahali pa Peramiho katika Tanzania

Majiranukta: 10°38′8″S 35°27′44″E / 10.63556°S 35.46222°E / -10.63556; 35.46222
Nchi Tanzania
Mkoa Ruvuma
Wilaya Songea Vijijini
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 15,503
Peramiho

Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka 2022, kata ilikuwa na wakazi wapatao 15,503 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 15,031 waishio humo. [2].

Abasia na parokia hariri

Inajulikana hasa kutokana na abasia ya wamonaki Wakatoliki Wabenedikto.

Abasia hiyo ilianzishwa kama kituo cha umisionari na P. Cassian Spiess O.S.B. aliyefika Peramiho mwaka 1898.

Mnamo mwaka 1931 Peramiho ilifanywa kuwa abasia na pia makao ya jimbo chini ya Abate-Askofu Gallus Steiger O.S.B..

Makao ya jimbo yalihamishiwa Songea mnamo mwaka 1969, na siku hizi kuna majimbo matatu (Jimbo kuu la Songea, Jimbo Katoliki la Njombe na Jimbo Katoliki la Mbinga) yaliyotokana na jimbo la zamani la Peramiho.

Peramiho kuna shule na hospitali nzuri pamoja na monasteri.

Pia ni makao makuu ya parokia ya Peramiho ambayo ina vigango vifuatavyo: Parangu, Lilambo, Likuyu, Mwanamonga, Litowa, Nakahuga, Sinai, Maposeni, Mdunduwalo na Morogoro.

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • Pugu Hadi Peramiho - kimehaririwa na P. Gerold Rupper, OSB, BPNP, Peramiho 1988, ISBN 9967 67 031 1

Viungo vya nje hariri

Marejeo hariri

  Kata za Wilaya ya Songea Vijijini - Mkoa wa Ruvuma - Tanzania  

Kilagano | Kizuka | Liganga | Lilahi | Litapwasi | Litisha | Magagula | Maposeni | Matimira | Mbinga Mhalule | Mpandangindo | Mpitimbi | Muhukuru | Ndongosi | Parangu | Peramiho


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Ruvuma bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Peramiho kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.