Posidi (kwa Kilatini: Possidius; aliishi karne ya 4 na ya 5) alikuwa Mberberi askofu wa Calama katika mkoa wa Numidia wa Dola la Roma (leo nchini Algeria)[1].

Possidius alikuwa askofu wa Calama, Numidia. Haya ni magofu ya mji huo wa kale.

Tangu kale Kanisa Katoliki linamheshimu kama mtakatifu, likiadhimisha sikukuu yake tarehe 16 Mei[2].

Maisha hariri

Rafiki wa Augustino wa Hippo kwa miaka 40 (Vita S. Augustini, xxxi), aliandika habari za kuaminika juu ya maisha yake pamoja na orodha ya vitabu alivyoviandika[3].

Akiwa padri katika monasteri ya Augustino (ibid., xii), alipofanywa askofu mnamo mwaka 397, alianzisha monasteri jimboni pia.

Alipambana na Wadonati hata mmojawao alijaribu kumuua. Hata hivyo yeye alidai wasiadhibiwe kwa kutozwa faini kubwa ("Vita", xii; Augustine, "Ep.", cv, 4; "Contra Crescon.", III, xlvi).

Mwaka 408 alinusurika tena kuuawa na Wapagani (Augustine, "Epp.", xc, xci, xciii).

Mwaka 409 aliteuliwa kwenda Italia pamoja na maaskofu wengine ili kuomba Kaisari awalinde Wakatoliki dhidi ya Wadonati, tena mwaka 411 aliteuliwa kuwa na mhadara na Wadonati.

Mwaka 416 alishiriki Mtaguso wa Milevi uliopinga Upelaji.

Wavandali walipovamia Afrika Kaskazini alikimbilia Hippo akashuhudia kifo cha Augustino (430).

Mwaka 437 anajulikana alikuwa bado hai, akiishi uhamishoni baada ya kufukuzwa na mfalme wa Wavandali Gaiseriko aliyekuwa Mwario.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/90177
  2. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
  3. *His Vita S. Augustini, composed before the capture of Carthage (439), is included in all editions of the works of Augustine, and also printed in Hurter's "Opusc. SS. Patr.". His indiculus ('small index') will be found in the last volume of Migne's edition of the works of Augustine and in the tenth volume of the Benedictine edition.

Vyanzo hariri

  • Ceillier, Hist. des auteurs ecclés., XII
  • Tillemont, Mémoires, XIII.
  • Weiskotten, Herbert T. (2008). The Life of Saint Augustine: A Translation of the Sancti Augustini Vita by Possidius, Bishop of Calama. Evolution Publishing, Merchantville NJ, U.S.A.  ISBN 1-889758-90-6 ISBN 9781889758909

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.