Rita wa Cascia (jina la kijiji hicho linatamkwa 'Kasha') alikuwa mjane wa Italia (jina la awali lilikuwa Margherita Lotti, Roccaporena, Perugia, Umbria, 22 Mei 1381 - Cascia, Perugia, 22 Mei 1457) aliyejiunga na shirika la wamonaki Waaugustino[1].

Mt. Rita akipewa na Yesu Kristo mmojawapo wa miba iliyomchoma kichwa siku ya Ijumaa Kuu.
Patakatifu pa Mt. Rita huko Roccaporena, Italia.

Papa Urban VIII alimtangaza mwenye heri mwaka 1626, halafu Papa Leo XIII akamtangaza mtakatifu tarehe 24 Mei 1900 kwa jina la "Mtakatifu wa mambo yasiyowezekana".

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 22 Mei[2].

Maisha hariri

Wazazi wa Rita walikuwa wanaitwa Antonio na Amati Loti. Katika kuzaliwa kwake Rita kulikuwa kwa pekee sana. Siku moja akiwa amelala kulitokea nyuki weupe walioonekana wakiingia na kutoka mdomoni mwake. Hii ilikuwa ishara ya utakatifu.

Rita alipenda sana kuwa sista lakini wazazi wake walimlazimisha awe mama wa familia. Kwa miaka mingi ilimbidi amstahimili mumewe mkatili hadi alipofaulu kumpatanisha na Mungu.

Baada ya kufiwa mume na watoto wake wote wawili alijiunga na monasteri.

Huko alijulikana kwa uvumilivu wake, kwa ukali wa malipizi yake na kwa ufanisi wa sala zake.[3]

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.