Rugaruga ilikuwa jina kwa aina mbalimbali ya askari wa kienyeji katika Afrika ya Mashariki wakati wa karne ya 19 na 20.

Rugaruga mnamo mwaka 1914 /15 wakiwa askari upande wa Wajerumani katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia; jina la picha katika kumbukumbu ni "Deutsch-Ostafrika, Hilfstruppen" (yaani "Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, askari wasaidizi")
Historia ya Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
This article is part of a series
Uendo
Historia ya Zanzibar
Afrika Mashariki 1800-1845
Ukoloni
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland
Mkwawa
Vita vya Maji Maji
Vita vikuu vya kwanza Afrika Mashariki
Tanganyika
Mapambano ya uhuru Tanganyika
Uhuru
Uhuru wa Tanganyika
Mapinduzi ya Zanzibar
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Julius Nyerere
Ujamaa
Tamko la Arusha
Vita vya Kagera
Ali Hassan Mwinyi
Benjamin Mkapa
Jakaya Kikwete
John Magufuli
Samia Suluhu Hassan

Tanzania Portal

Rugaruga wa Mirambo hariri

Jina "Rugaruga" lilikuwa maarufu tangu miaka ya 1860 kama jina la askari wa Mtemi Mirambo aliyekuwa mtemi wa Wanyamwezi katika magharibi ya Tanzania ya leo.

Mirambo aliwahi kutajirika kama mfanyabiashara kwa njia ya misafara kati ya pwani ya Bahari Hindi na Kongo. Alitumia sehemu kubwa ya utajiri wake kujenga jeshi la binafsi. Kwa kusudi hii alinunua bunduki aina ya magobori na kukusanya vijana wengi walioitwa "rugaruga". Kwa kawaida vijana hao walikuwa wanaume walioishi bila ukoo na bila familia waliowahi kutoroka kwenye hali ya utumwa au kuwa wapagaji wa misafara.[1] Mirambo aliwapokea na kuwapa silaha na kwa njia hii alishinda maadui hadi kuwa mtemi mkuu wa Waynamwezi kuanzia 1860 hadi kifo chake mnamo 1884. Rugaruga hawa walihofiwa kote na Mirambo aliweza kupanusha eneo lake kwa msaada wao. Inasemekana ya kwamba kabla ya mapigano walipewa pombe na banghi kwa kusudi ya kuongeza ukali na kupunguza hofu yao ya kifo.

Rugaruga kama wanajeshi wa kienyeji hariri

Kutokana na askari wa Mirambo jina la "Rugaruga" lilijulikana kote likawa kawaida kwa askari wa watawala wengi. Wajerumani walipotwaa eneo la Afrika ya Mashariki ya Kijerumani walikuta neno hili mahali pengi lilikuwa njia ya kutaja askari au mapolisi wa kienyeji.[2]

Wakati wa ukoloni ilikuwa pia jina la wasaidizi waliotolewa na vijiji au machifu kwa msaada wa jeshi rasmi la koloni. Kwa mfano wakati wa vita ya maji maji vikosi wa jeshi la kikoloni viliongezeka vikundi vya "rugaruga" walioteuliwa na machifu kuwasaidia kukandamiza upinzani wa maji maji. Wale rugaruga walikuwa tofauti na askari Waafrika ndani ya jeshi la kikoloni waliovaa sare rasmi wakiteuliwa na kufundishwa kufuatana na utaratibu wa Kijerumani.[3] Kwa maana hii rugaruga walipatikana upande wa Wajerumani na pia upande wa Waingereza huko kenya.

Polisi wa machifu wakati wa koloni hariri

Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia neno "rugaruga" ilikuwa jina la mapolisi na askari waliokuwa wasaidizi wa machifu ndani ya utawala wa kikoloni wa Kiingereza nchini Tanganyika na Kenya.[4]

Marejeo hariri

  1. John Iliffe: A Modern History of Tanganyika. Cambridge University Press, Cambridge 1979, uk. 64
  2. Linganisha maelezo kwenye kamusi ya Carl Velten: Suaheli Wörterbuch. I. Teil Suaheli – Deutsch, Berlin 1910, makala: Rugaruga
  3. Makala Rugaruga katika Kamusi ya Koloni za Kijerumani (1920). Berlin 1920.
  4. linganisha Frederick Johnson (Hrsg.): A Standard Swahili – English Dictionary. Oxford University Press, 1939 (reprint 2000), makala: Rugaruga