Severino wa Settempeda

Severino wa Settempeda (Settempeda, leo San Severino Marche, Italia 470 hivi - Settempeda, 545) alikuwa Mkristo ambaye, alipofiwa wazazi wake, aliamua pamoja na ndugu yake Viktorini wa Camerino kuwagawia maskini urithi wao mkubwa na kwenda kuishi upwekeni kwenye Mlima Nero.

Mt. Severino katika mavazi ya kiaskofu alivyochorwa na Vittore Crivelli, 1482 hivi.

Papa Vigili alimfanya yeye askofu wa Settempeda na Viktorini askofu wa Camerino (Italia ya Kati)[1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Mei[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/90943
  2. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.