Sherehe kuu 12 (kwa Kigiriki: Δωδεκάορτον, Dodekaorton) za Makanisa ya Kiorthodoksi, tukiacha Pasaka iliyo sikukuu ya sikukuu zote, zinawaadhimisha Yesu Kristo (8) pamoja na Bikira Maria (4).[1]

Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki

Ni hizi zifuatazo:

  1. 21 Septemba [O.S. 8 Septemba], Kuzaliwa kwa Mama wa Mungu
  2. 27 Septemba [O.S. 14 Septemba], Kutukuka kwa Msalaba
  3. 4 Desemba [O.S. 21 Novemba], Mama wa Mungu kutolewa hekaluni
  4. 7 Januari [O.S. 25 Desemba], Kuzaliwa kwa Kristo/Krismasi
  5. 19 Januari [O.S. 6 Januari], Ubatizo wa KristoTheofania, inayoitwa pia Epifania
  6. 15 Februari [O.S. 2 Februari], Yesu kutolewa hekaluni
  7. 7 Aprili [O.S. 25 Machi], Kupashwa Habari Maria
  8. Jumapili kabla ya Pasaka — Kuingia Yerusalemu Jumapili ya Matawi au ya Mitende au ya Maua
  9. Siku arubaini baada ya Pasaka — Yesu Kristo Kupaa Mbinguni
  10. Siku hamsini baada ya Pasaka — Pentekoste
  11. 19 Agosti [O.S. 6 Agosti], Yesu Kugeuka Sura
  12. 28 Agosti [O.S. 15 Agosti], Kulala kwa Mama wa Mungu

Mbali ya hizo, Waorthodoksi wana sherehe nyingine tano zinaazohesabiwa kuwa kuu: Tohara ya Kristo 14 January [O.S. 1 January], Kuzaliwa kwa Yohane Mbatizaji 7 Julai [O.S. 24 Juni], Watakatifu Petro na Paulo 12 July [O.S. 29 June], Kukatwa Kichwa kwa Yohane Mbatizaji 11 Septemba [O.S. 29 Agosti], na Ulinzi wa Mama wa Mungu 14 Oktoba [O.S. 1 Oktoba].[2]

Tanbihi hariri

  1. Mother Mary and Ware, Kallistos, "The Festal Menaion", p. 41. St. Tikhon's Seminary Press, 1998.
  2. Moscow Typikon, 1904, reprinted Graz, Austria, 1964

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sherehe kuu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.