Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Sikukuu ya amri ni msamiati unaotumika katika Kanisa Katoliki kutaja sikukuu ambayo waumini wake "wanapaswa kushiriki Misa; pia waepe kufanya kazi na shughuli zinazozuia ibada kwa Mungu na kuvuruga furaha maalumu ya siku ya Bwana au pumziko la akili na mwili linalohitajika" (kan. 1247).

"Anatimiza wajibu wa kushiriki Misa muumini anayeihudhuria popote inapoadhimishwa kadiri ya liturujia Katoliki ama siku yenyewe ya sikukuu, ama jioni mwa jana yake" (kan. 1248)

Amri hiyo inafafanua namna ya Mkatoliki kutekeleza amri ya tatu ya Mungu na inakumbushwa katika katekisimu kama ya kwanza kati ya zile tano kuu.

Wakatoliki wa Mashariki wana sheria zinazofanana na hizo (kan. 880-881).

"Siku ya Dominika, ambapo fumbo la Pasaka linaadhimishwa, kutokana na mapokeo ya Mitume ni lazima ishikwe katika Kanisa lote kama sikukuu asili ya amri. Vilevile inabidi zishikwe siku za Kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, Epifania, Kupaa Bwana, Mwili na Damu takatifu sana ya Kristo, Mtakatifu Maria Mama wa Mungu, Kukingiwa dhambi ya asili na Kupalizwa kwake mbinguni, mtakatifu Yosefu, watakatifu mitume Petro na Paulo, na hatimaye Watakatifu wote. Hata hivyo, Baraza la Maaskofu linaweza, kwa idhini ya Ukulu wa Kitume, kufuta au kuhamishia Dominika baadhi ya sikukuu za amri" (kan. 1246).

Tanbihi hariri


Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sikukuu ya amri kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.