Sikukuu ya msalaba

Sikukuu ya msalaba ni adhimisho la liturujia ya madhehebu mbalimbali ya Ukristo wa mashariki na vilevile ya Ukristo wa magharibi, ingawa tarehe zinatofautiana.

Picha takatifu ya Gury Nikitin, 1680 kuhusu sikukuu ya kutukuka kwa msalaba (kutoka Yaroslavl, leo katika Tretyakov Gallery, Moscow, Urusi).

Sikukuu inaitwa kwa Kigiriki Ὕψωσις τοῦ Τιμίου καὶ Ζωοποιοῦ Σταυροῦ[1] ("Kuinuliwa kwa Msalaba wenye kuheshimiwa na kuleta uzima"), kwa Kirusi Воздвижение Креста Господня na kwa Kilatini Exaltatio Sanctae Crucis ("Kutukuka kwa Msalaba Mtakatifu"). Walutheri na baadhi ya Waanglikana wanaiita Holy Cross Day ("Siku ya Msalaba Mtakatifu"), pengine Feast of the Glorious Cross ("Sikukuu ya Msalaba Mtukufu").

Lengo ni kutukuza chombo cha wokovu wa binadamu wote kilichotumiwa na Mungu kadiri ya imani ya dini hiyo, yaani Yesu Kristo aliyeuawa juu ya msalaba huko Yerusalemu mwaka 30 hivi.

Wakati Ijumaa Kuu inalenga zaidi mateso ya Yesu, Mwanakondoo wa Mungu aliyeondoa dhambi ya ulimwengu, sikukuu hiyo inashangilia utukufu wa fumbo hilo, ambalo Mtume Paulo alilitangaza kuwa fahari yake pekee (Gal 6:14).

Kabla yake, Yesu mwenyewe alizungumzia "kuinuliwa" kwake (Yoh 3:14-15), akimaanisha kuinuliwa msalabani na mbinguni vilevile. Hivyo alidokeza kwamba msalaba wake haukuwa aibu, bali hasa utukufu.

Adhimisho la tarehe 14 Septemba hariri

Hadithi zilizoenea sana zinadai mwaka 326 msalaba halisi wa Yesu uligunduliwa na mtakatifu Helena wa Konstantinopoli, mama wa Kaisari Konstantino I, alipohiji Yerusalemu. Hapo kanisa la Kaburi na Ufufuo wa Yesu lilijengwa mahali penyewe, kwa amri ya Helena na Konstantino, na sehemu ya msalaba iliachwa huko, ila sehemu nyingine zilipelekwa Roma na Konstantinopoli.

Tarehe 14 Septemba ndiyo siku ya pili ya kutabaruku kanisa hilo mwaka 335[2] na ndiyo siku ya adhimisho lake katika Kanisa Katoliki la Kilatini[3].

Tanbihi hariri

  1. "Jerusalem Patriarchate". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2013-09-15. Iliwekwa mnamo 2016-09-11. 
  2. [1] "Sanctuary Holy Sepulchre", Retrieved 2014-04-30
  3. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sikukuu ya msalaba kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.