Skopje (Kimasedonia: Скопје; tamka: Skopye) ni mji mkuu pia mji mkubwa wa Jamhuri ya Masedonia Kaskazini. Zaidi ya robo ya wakazi wote wa nchi hiyo kukaaa hapa.

Daraja la kale juu ya mto Vardar.

Skopje ni kitovu cha uchumi, utamaduni na siasa wa nchi.

Anwani ya kijiografia ni 42°0′N 21°26′E.

Mto Vardar hupita katika mji.

Historia hariri

  • Skopje ni mji wa kale iliyojulikana tangu zamani za Dola la Roma kwa jina la "Scupi". Iliharibiwa na tetemeko la ardhi mwaka 518.
  • katika karne ya 10 ilikuwa mji mkuu wa kwanza wa Bulgaria
  • Katika karne ya 14 Waserbia walitwaa Skopje. Mwaka 1345 mfalme wa Serbia Stefan Uroš IV. Dušan alijitangaza kuwa "Kaisari wa Waserbia na Wagiriki" mjini Skopje. Skopje ikawa mji mkuu wa dola la Serbia.
  • Kuanzia 1392 Skopje ilitwaliwa na Waturuki Waosmani ikaitwa nao Üsküp kwa miaka 500 iliyofuata.
  • 1555 mji uliharibiwa tena na tetemeko la ardhi.
  • 1913 mji ulitwaliwa na jeshi la Serbia katika vita ya pili ya Balkani na kuwa sehemu ya Serbia hadi 1945.
  • Tangu 1945 Skopje ikawa mji mkuu wa jimbo (jamhuri ya shirikisho) la Masedonia ndani ya Yugoslavia.
  • 1963 mji uliharibiwa tena na tetemeko kali la ardhi.
  • tangu 1991 Skopje imekuwa mji mkuu wa nchi huru ya Jamhuri ya Masedonia Kaskazini.

Watu mashuhuri waliozaliwa Skopje hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Skopje kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.