Swalah (au al-Ṣalāt; kwa Kiarabu: الصلاة) ni ibada muhimu zaidi ya Waislamu ambayo inajulikana katika Qur'an na hadithi, kama vile nguzo ya dini, kupaa kwa roho, kutakasa nafsi, matendo ya kwanza ambayo yataulizwa kuhusu Siku ya Hukumu, na ni sharti la kukubalika kwa matendo mengie mema. Pia imetajwa katika vyanzo hivi kwamba sala huzuia dhambi, huweka mpaka kati ya muumini na kafiri, na huondoa kiburi.

Sehemu ya mfululizo wa makala juu ya

Uislamu

Imani na ibada zake

Umoja wa Mungu
Manabii
Misahafu
Malaika
Uteule
Kiyama
Nguzo za Kiislamu
ShahadaSwalaSaumu
HijaZaka

Waislamu muhimu

Muhammad

Abu BakrAli
Ukoo wa Muhammad
Maswahaba wa Muhammad
Mitume na Manabii katika Uislamu

Maandiko na Sheria

Qur'anSunnahHadithihttps://sw.wikipedia.org/w/index.php?search=Ali%20ibn%20Abu%20Talib&title=Maalum%3ATafuta&wprov=acrw1_2
Wasifu wa Muhammad
Sharia
Elimu ya Sheria za KiislamuKalam

Historia ya Uislamu

Historia
SunniShi'aKharijiyaRashidunUkhalifaMaimamu

Tamaduni za Kiislamu

ShuleMadrasa
TauhidiFalsafaMaadili
Sayansi
SanaaUjenziMiji
KalendaSikukuu
Wanawake
ViongoziSiasa
Uchumi
UmmaItikadi mpyaSufii

Tazama pia

Uislamu na dini nyingine
Hofu ya Uislamu

Swala imekua wajibu kwa Waislamu kabla ya Hijra ya Mtume Muhammad. Mwanzoni, Waislamu walifanya sala kuelekea Masjid al-Aqsa huko Yerusalemu (al-Quds), lakini kuanzia mwaka wa pili baada ya Hijra/623-4, walitakiwa kuswali wakielekea Kaaba huko Makka.

Mbali ya mambo yake ya kiroho, sala inajulikana kama kauli mbiu muhimu zaidi ya Uislamu. Sala ya Ijumaa na sala za jamaa zinaingia katika kipengele muhimu cha kijamii cha ibada hii.

Mbali ya kuwa ibada ya lazima, kuna salah nyingi ambazo zimetajwa katika hadithi kuwa zina manufaa sana kwa ulimwengu huu na maisha ya baadaye. Miongoni mwa sala hizo muhimu zaidi ni sala za usiku na sala ya Nafila ambayo inaambatana na wajibu.

Istilahi hariri

Ni neno la Kiarabu "صلاة" (ṣalāt) limetokana na mzizi "ص ل و" ambayo inamaanisha sala na fomu yake ya wingi ni "salawat". Sala pia hutumiwa kwa maana ya du'a (maombi) katika baadhi ya aya za Qur'an.

Umuhimu wa swalah hariri

Sala imetajwa mara tisini na nane katika Qur'an. Ina umuhimu mkubwa sana ambao umetajwa, mbali ya imani, salah ni kama matendo ya kwanza ya kiibada ya mtu binafsi na ya pamoja katika aya nyingi. Katika Qur'an swalah imetajwa kama kizuizi dhidi ya kutenda dhambi, pia ni njia ya kufikia ukombozi, ni msaada wakati wa kukabiliana na matatizo, ni moja ya amri muhimu za Mungu kwa manabii, na ni moja kati ya masisitizo makubwa ya manabii hasa kwa familia zao.

Imesemwa katika Qur'ani kwamba waunguaji wa mwanzo katika wakazi wa Jehanum, ni wale ambao hawakuswali swala zao katika maisha yao hapa duniani. Pia, watu ambao walikuwa na uzembe juu ya sala zao wanasemekana kuwa ni sawa na wale wanaoikana dini.

Sala ina nafasi ya ajabu katika maneno na matendo ya Mtume. Kuna zaidi ya hadithi 11,600 kuhusu sala katika vitabu wasa'il al-Shi'a na Mustadrak al-wasa'il, kuonyesha umuhimu wake wa pekee miongoni mwa Maimamu 12 wa Shia.

Kuna maneno na vifungu mbalimbali vinavyoelezea swalah katika hadithi:

  • Nguzo ya dini
  • Matendo ya kiibada ya kwanza na ya lazima ya Mungu
  • Nuru ya watu wachaMungu
  • Ishara ya imani
  • Njia bora zaidi ya kumkaribia Mwenyezi Mungu
  • Ufunguo wa Mbinguni
  • Mng'aro katika macho ya Mtume
  • kiwakilishi cha Uislamu
  • Moja ya njia bora zaidi siku ya hukumu
  • Ibada ya kwanza ambayo itaulizwa Siku ya Hukumu
  • Kigezo cha kutambua mfuasi halisi wa uislamu
  • Mwenzi kwa ajili ya mwanadamu katika giza la kaburi
  • Njia ya kutimiza matakwa ya mtu
  • Njia ya kusafisha roho ya mtu
  • Ngome dhidi ya Shetani
  • Ufunguo wa matendo mengine yote mema.
  • Kuacha kiburi
  • Kumalizika kwa dhambi
  • Njia ya kumfukuza Shetani
  • Njia ya kuangaza nyumba za waja kwa mwongozo/nuru ya Mwenyezi Mungu
  • Njia ya kuzuia majanga
  • Njia ya kushinda huzuni na unyonge
  • Kibali cha kupita katika Sirat (daraja/njia nyembamba siku ya hukumu).

Adhabu kali na matokeo yake yametajwa kwa kupuuza au kutoswali swala za wajibu kama vile:

  • Sababu ya kuwa mkaazi wa Jahannamu
  • Ishara ya unafiki
  • Majuto katika maisha ya barzakh
  • Kunyimwa maombezi/msamaha
  • Kutokua na baraka katika maisha
  • Kutokua na baraka katia kipato na mali
  • Uso wa giza
  • Kutokuwa na malipo kwa matendo mema mengine
  • Kifo chaa dharau
  • Kutotimiziwa matakwa na dua
  • Kutokubaliwa kwa dua za watu wengine kwa mtu asiyeswali
  • Giza na shinikizo kaburini
  • Adhabu kali na hukumu kali siku ya kiyama
  • Mungu hammbariki asiyeswali.

Hitoria ya Swalah hariri

Swalah ni ibada ambayo kila dini imeianzisha, ingawa kumekuwa na aina tofauti kwa sababu ya tofauti katika dini. Baadhi ya swala za Manabii, wakiwa ni pamoja na Ibrahimu, Isma'il, Ishaq, Musa, Zekaria, Issa, Shu'ayb, na Luqman zimetajwa katika Qur'an. Katika hadithi, sala ya Adamu pamoja na manabii wengine wengi zinaonyeshwa.

Kwa mujibu wa Qur'an, swalah haijabainishwa kwa wanadamu tu. Kila kiumbe mbinguni au ardhini kina swalah yake maalum:

"Je, hukuona ya kuwa Mwenyezi Mungu ametukuzwa na kila mtu mbinguni na ardhini, na ndege wanaeneza mbawa zao. Kila mmoja anajua sala yake na utukufu wake, na Mwenyezi Mungu anajua zaidi wanayoyatenda".

Katika miaka ya mwanzo ya Uislamu, wakati mtume Muhammad anaeneza dini kwa siri, alikuwa akiswali pamoja na Imam Ali na Bibi Khadija. Lakini wajibu wa maombi ya kila siku ulitangazwa na Mungu katika mi'raj (usiku wa kupaa kwa mtume), karibu miezi kumi na nane kabla ya kuhama. Sala hizo zilikuwa zikiswaliwa rakaa mbili mbili na rakaa nyingine saba ziliongezwa kwao katika mwaka wa kwanza baada ya kuhamia Makka, kwa hiyo, aina ya mwisho ya swalah ilianzishwa.

Aina za Swalah hariri

Swala ni aina ya ibada na hakuna mtu ana haki ya kufanya swala ambayo haijakuwepo katika dini: jambo hili ni marufuku katika Uislamu. Kuna aina zifuatazo za swalah:

Swala za Lazima hariri

Swalah za lazima zinaweza kugawanyika katika sehemu kuu mbili:

Swala za Kila Siku hariri

Sala za kila siku ni sala tano na zina jumla ya raka'a 17, hapa kuna majina ya swalah hizo na wakati wake:

  • Swala ya Fajr (sala ya alfajiri): Ina rak'a mbili, wakati wake ni kuanzia alfajiri (fajr) hadi jua linapochomoza.
  • Swala ya Dhuhr (sala ya adhuhuri): Ina rak'a nne, wakati wake ni baada ya dhuhr (adhuhuri) mpaka maghrib (linapozama jua).
  • Sala ya asr (sala ya alasiri): Ina rak'a nne, wakati wake ni baada ya swala ya adhuhuri mpaka maghrib (jua kuzama).
  • Sala ya Maghrib: Ina rak'a tatu wakati wake ni jua kuzama ambapo wekundu wa anga ya mashariki utapita juu ya kichwa cha mtu hadi usiku wa manane.
  • Swala ya Isha: Ina rak'a nne, na wakati wake ni baada ya sala ya maghrib hadi usiku wa manane.

Wakati wa kusafiri, sala zinazojumuisha rak'a nne hupunguzwa katika na kuswaliwa rak'a mbili (swala ya msafiri)

Swalah za Lazima ya Mara kwa Mara hariri

  • Swala ya Ayat (sala ya ishara): Ina rak'a mbili na ruku tano katika kila rak'a; Ni swala inayoswaliwa iwapo mojawapo ya ishara/matukio haya yatatokea: kupatwa kwa mwezi, kupatwa kwa jua (sehemu au jumla), tetemeko la ardhi, nk.
  • Sala ya Qadha (sala ya fidia): kama mtu hakuswali swala yake wakati mda wa swala ulipoiungia, mtu huyo atakua amefanya dhambi na lazima aswali swala hiyo baadaye kwa nia ya fidia. Ubora wa sala ya qada ni sawa na sala iliyokosa isipokuwa kwa wakati.
  • Swala ya Mazishi: Huswaliwa pamoja na takbira tano na dhikr maalum kati ya kila takbira mbili wakati watu wakiwa wamesimama, bila rukuu wala sijda, hufanyika kwa Waislamu waliokufa kabla ya mazishi yao.

Swala zilizopendekezwa/ Swalah za sunna hariri

Kwa kuwa sala ni matendo mazuri zaidi na kamilifu ya ibada, kuna swala nyingi za kiimani pamoja na lazima kwa wale wenye shauku/wenye kutaka kuswali swala hizo (sio za lazima). Haiwezekani kupata fursa ya kidini bila ya kuswali swala hizi, maelekezo ya swala hizi mengi yanapatikana katika Mafatih al-jinan. Mfano wa swala hizo ni:

  • Sala za Nafila: Ni sala muhimu zaidi na zilizopendekezwa. Nafila ni sala zinazofanywa kabla (au baada) ya sala za kila siku.
  • Sala ya usiku ni sehemu mashuhuri ya sala za Nafila na pia ni moja ya sala muhimu zaidi. Inaswihi sana na ni yenye thamani kubwa ambayo imekuwa ni swala ya lazima kwa Mtume Muhammad, na imependekezwa sana katika hadithi.

Sala nyingine zilizopendekezwa ni Sala ya Eid, Sala ya Ja'far al-Tayyar, Sala kwa ajili ya msaada na mengine mengi.

Kanuni za swala hariri

Kabla ya kuanza kuswali, maandalizi lazima yafanywe. Kwanza tohara yote inapaswa kupatikana kupitia kufanya wudu, ghusl, au tayammum kulingana na hali. Kisha, mtu lazima aelekee qibla (Ka'ba huko Makka) akiwa na mwili safi pamoja na nguo zake.

Vipengele vya lazima vya sala ni kumi na moja:

  1. Niyya (kutia nia moyoni/kwa sauti)
  2. Qiyam (Kisimamo/kusimama)
  3. Takbirat al-Ihram (Kuhirimia swala/kusema "Allah-u akbar")
  4. Ruku' (kuinama)
  5. Sujud (kusujudu)
  6. Qira'a (kusoma qur'an, sura el Fat'ha na nyingine kkatika raka'a mbili za mwanzo)
  7. Dhikr (kusoma dhikr/kumtaja m/mungu wakati wa kuinama na kusujudu)
  8. Tashahhud (Kusoma shahada)
  9. Salam (Kutoa salamu)
  10. Tartib (utaratibu/mpangilio wa vitendo vya swala)
  11. Muwalat (vitendo lazima viwe katika mtiririko unaoendelea bila kupumzika kwa muda mrefu katikati)

Kanuni tano za kwanza ni sehemu muhimu/lazima za swala (rukn). Kuna tofauti kati ya vipengele muhimu (rukn) na visivyo muhimu: Ikiwa mtu hafanyi vipengele muhimu ama kwa bahati mbaya au kwa kusudi, sala ni batili. Lakini kuhusu vipengele visivyo vya lazima, ikiwa mtu hafanyi kwa kusudi sala ni batili na ikiwa mtu anavisahau kwa bahati mbaya sala ni sahihi.

Jinsi ya kuswali kwa utaratibu wa Kishia hariri

Simama ukielekea qibla na utie nia kwa utulivu moyoni, ijapokuwa kutamka nia sio lazima, ila ni bora kuitamka nia yako kwa mfano, "Ninanuia kuswali swala ya Alfajir raka'a mbili kwa ajili ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu mtukufu".

Rak'a ya kwanza hariri

  • Sema takbirat al-ihram: Inua mikono yako juu mpaka karibu na masikio yako na usemee: "Allah-u akbar", maana yake: Mwenyezi Mungu ndiye mkubwa zaidi).
  • Anza kusoma sura al-Hamd, baada ya hapo, uko huru kusoma sura yoyote kamili unayotaka, kama sura al-tawhid.
  • Nenda ruku' (Inama) na usema dhikr yake: سُبْحانَ رَبّیَ الْعَظیمِ وَ بِحَمْدِه (tafsiri yake: "subhan-a rabbi-a l-'azim-i wa bi-hamdih"; maana yake: Utukufu ni wa m/mungu, mkubwa, Na ninamsifu) au badala yake, unaweza kusema mara tatu سُبْحانَ الله (tafsiri yake: "subhan Allah"; maana yake: kuinuliwa ni kwa Mwenyezi Mungu).
  • Baada ya hapo simama tena na kisha, nenda sijda (Kusujudu): weka kichwa chako chini na useme dhikr ya sujud سُبْحانَ رَبّیَ الناَعلی وَ بِحَمْدِه (Tafsiri: "Subhan-a rabbi-a l-a'la wa bi-hamdih; maana: kuinuliwa kuwa bwana wangu, wa juu, na mimi namsifu), au kusema mara tatu سُبْحانَ الله (sub-hana llah)Kisha, kaa magotini mwako kwa sekunde chache na ufanye sujud tena na urudie dhikri ile ya sujudu.
Rak'a ya pili hariri
  • Baada ya sujud ya pili ya rak'a ya kwanza, simama tena usome sura al-Fatiha na sura nyingine ya Qur'ani Tukufu.
  • Baada ya kukariri Fatiha na sura nyingine oqunut: inua mikono yako na kuweka mikono yako mbele ya uso wako, kugeuzaa viganja vyako vitazame anga, na weka mikono na vidole karibu pamoja. Katika hali hii, unaweza kusema du'a yoyote unayoitaka.رَبَّنا آتِنا فِی الدُّنْیا حَسَنَةً وَ فِی الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَ قِ, Tafsiri yake: "Rabbana atina fi l-dunya hasanat-an wa fi l-akhirat-i hasanat-an wa qina 'adhab-a l-nar"; maana yake: "Mola wetu, tupe mema katika dunia hii na mema katika Akhera, na utuokoe na adhabu ya Moto" hata hivyo kusema qunut ni hiyari.
  • Baada ya Qunut, unapaswa kufanya ruk'u sawa na rak'a ya kwanza.
  • kisha kusimama na tena kusujudu mara mbili.
  • Kisha, kaa na usome tashahhud:
                   اَشْهَدُ اَنْ لااِلهَ اِلاَّ اللّهُ وَحْدَهُ لاشَرِیكَ لَهُ، وَاَشْهَدُ اَنَّ مُحَمَداً عَبْدُهُ وَ رَسُولُه، اَلّلهُمَّ صَلِّ عَلی مُحَمَّد وَ آلِ مُحَمَّد

(Tafsiri yake: "Ashhad-u an la ilah-a illa Allah, wa ashhad-u anna Muhammad-an abduh-u wa rasuluh, Allahumma sall-i ala Muhammad-in wa al-i Muhammad; Maana: Ninashuhudia kwamba hakuna Mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu ambaye ni mmoja bila mshirika yeyote, na ninashuhudia kwamba Muhammad ni mtumishi Wake na Mtume Wake, Ewe Allah ambariki Muhammad na familia ya Muhammad)

  • Kama swala hiyo ni ya rakaa mbili katika rakaa hii ya pili baada ya shahada utasoa salaam/ utamaliza swala kwa kutoa salaam.nayo ni;
               اَلسَّلامُ عَلَیْكَ اَیُّهَا النَّبِیُّ وَ رَحْمَةُ اللّهِ وَ بَرَکاتُهُ، اَلسَّلامُ عَلَیْنا وَ عَلی عِبادِ اللّهِ الصّالِحینَ، اَلسَّلامُ عَلَیكُمْ وَ رَحْمَةُ اللّهِ وَ بَرَکاتُهُ 

(Tafsiri yake: al-salam-u 'alayk-a ayyuha l-Nabiy-yu wa rahmat-u l-Allah-i wa barakatuh, al-salam-u 'alayna wa 'ala'ibad-i l-Allah-i l-salihin, al-salam-u 'alaykum wa rahmat-u l-Allah-i wa barakatuh; maana yake: amani iwe juu yako Ewe Mtume, na rehema za Mwenyezi Mungu na fadhila zake, amani iwe juu yetu na juu ya waja wema wa Mwenyezi Mungu, amani iwe juu yenu nyote, na rehema za Mwenyezi Mungu na fadhila zake.

Kama Sala ni ya rak'a mbili itakua imemalizika baada ya salaam.

Rak'a ya tatu na ya nne hariri
  • Ikiwa sala ni ya rakaa tatu au nne, lazima usimame baada ya tashahhud, na badala ya kusoma sura al-Fatiha na sura nyingine, unapaswa kusoma tasbihat al-arba'a (tasbihs nne):
                                سُبْحانَ اللّهِ وَ الْحَمْدُ لِلّهِ وَ لاإلهَ اِلّا اللّهُ وَ اللّهُ أكْبَر

(Tafsiri yake: subhan Allah wa l-hamd-u li-Allah wa la ilah-a illa Allah wa Allah-u akbar; maana ya ke: kuinuliwa kuwa Mwenyezi Mungu na sifa ni za Mwenyezi Mungu na hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ndiye Mkubwa zaidi.)

  • Ifuatayo, ni zamu ya ruku' na sijda mbili.

Ikiwa swala ni ya rakaa tatu, Tashahhud na Salam lazima zisomewe baada ya sujuds mbili kwenye rakaa ya tatuu. Lakini kama sala ina rakaa nne, lazima usimame baada ya sijda mbili za rakaa ya tatu na kusoma tasbihat al-arba'a, na baada ya hapo utaruku na kusujudu mara mbili, utasoma tashahhud na salam.

Sala zote za sunna/zisizo za lazima ni rakaa mbili mbili, isipokuwa kwa sala ya mwisho ya sala ya Usiku (Sala ya Witr) na sala ya A'rabi. Kwa mfano, moja ya mazoea katika Eid al-Ghadir ni sala ya sunna yenye raka'a 12, ni lazima iswaliwe kama sala sita, kila moja ikiwa na rakaa mbili mbili.

Lugha ya swalah[1] hariri

Waislamu wote hufanya ibada zao za kidini na salah zote, ikiwa ni pamoja na sala za kila siku mara tano, kwa Kiarabu. Katika kipindi cha sala hizi, baadhi ya Aya za Qur'an na sentensi nyingine, zimetamkwa ili kuonyesha Ukuu na Utukufu wa Mwenyezi Mungu, Muumba, na unyenyekevu na upungufu wa wanadamu, viumbe.

Hii inafanywa kwa maneno sawa na Waislamu wote, Waarabu na wasio Waarabu, hata na wale ambao hawaelewi Kiarabu. Mfumo huo wa sala katika lugha moja ya kawaida ulikuwa unatekelezwa wakati wa maisha ya Mtume wa Uislamu na umeendelea baada yake kwa zaidi ya miaka 1400. Katika kila nchi, Waislamu wamekuwa wakisali kwa lugha ya Kiarabu.

Swali ambalo mara kadhaa huulizwa ni kwa nini Muislamu anapaswa kuswali tu kwa lugha ya Kiarabu na sio lugha yake mama?

Inaweza kuonekana kuwa na mantiki kwamba kila Muislamu aombe kwa lugha yake mwenyewe, ili aweze kuelewa kile anachosema; lakini kuna hoja kali ya kwa nini ni lugha moja tu itumike kwenye ibada/salah za kiislam, tena iwe ni Kiarabu. Hoja hizo ni kwamba:

Kiarabu ni lugha ya kina na kubwa/pana hariri

Ni ukweli unaotambuliwa na wanaisimu kwamba lugha ya Kiarabu ina uwezo bora wa kuelezea mawazo mapana na ya kina na kuelezea masomo muhimu kwa maneno mafupi na sahihi, hata kuwasilisha maneno ya kina ya kiroho, kimaadili kwa namna nzuri sana. Kwa hiyo uchaguzi wa Kiarabu kwa ajili ya sala za Kiislamu si ajabu.

Veccia Vaglieri, mtaalamu wa Kiitalia katika Chuo Kikuu cha Napoli, anaandika katika kitabu chake juu ya Maendeleo ya Uislamu, kwamba katika kazi yoyote ya fasihi ulimwenguni hakuna kazi yoyote inayoweza kupatikana sentensi zenye maana kubwa sana kwa maneno mazuri isipokuwa katika Qur'an; na kina hicho cha maana kinavikwa taji na lugha ya ufasaha kama hiyo.

Marehemu George Bernard Shaw, wakati wa majadiliano yake juu ya Uislamu huko Mombasa mwaka 1943 alisema: "Pia ninavutiwa sana na maneno ya kukubalika na ya kuvutia ya Qur'an. Ni neema gani na uzuri unaoonyeshwa kipengele ambacho kinaelezea "eneo la kutisha la uwanja wa siku za majuto/maangamizi, kwa kushughulika na mauaji ya watoto wachanga", kwa kiasi kikubwa huacha swali, 'Kwa uhalifu gani uliokua?' kwa mtoto asiye na hatia ambaye alizikwa akiwa hai au kuuawa. Kwa maoni yangu hii ni njia bora zaidi ya kujenga hisia za kudumu katika akili za watu."

Profesa Arbury, mwanachuoni anayejulikana sana Chuo Kikuu cha Cambridge, anasema kuwa hakuna lugha iliyo na uwezo wa kuweka sentensi fupi, kwa mfano neno من (Min) (ambalo linarudiwa mara tano katika aya ya Qur'an) bila kuvuruga ufasaha na kufikisha maana yake, isipokuwa lugha ya Kiarabu ambayo imechaguliwa na Mwenyezi Mungu itumike katika Qur'an kwaajili ya kufikisha ujumbe wa Uislamu.

Kuimarisha udugu wa Kiislamu hariri

Kuswali kwa Kiarabu huimarisha udugu wa Kiislamu na kusisitiza tabia ya ulimwengu wote ya Uislamu. Uislamu umekuja kwa ajili ya jamii nzima ya binadamu. Ni ukweli kwamba Jumuiya za Kiislamu duniani, kama jamii nyingine zote, huzungumza lugha na lahaja nyingi tofauti. Wakati huohuo inapaswa kufahamu kwamba maisha yetu leo yanachukua haraka tabia ya kimataifa. Umbali kati ya sehemu mbili za ulimwengu sasa umepungua kwa kiasi kikubwa. Katika kila sehemu utapata Waislamu wanaozungumza lugha tofauti.

Fikiria Muislamu ambaye ni Mwingereza anayekwenda China na kupita mitaani. Ghafla anasikia sauti inayosema 'ching-chang-chung' ambayo, tuchukulie kwa mfano maana yake ni 'Allahu Akbar' yaani - Mungu ni Mkuu. Bila shaka mgeni hawezi kuelewa kwamba ni wito wa sala ya Kiislamu na angekosa fursa ya kuswali pamoja na watu wa eneo hilo. Kwa bahati mbaya, misikiti nchini China haifanani na kuonekana kama ile ya Ulaya au nchi nyingine za Mashariki na hawana minara. Kinyume chake, kama Mchina anasafiri nje ya nchi ambako watu wanaswali kwa lugha yao ya ndani, hangeweza kuielewa na kushiriki katika hilo.

Sayyid Sa'eed Akhtar Rizvi, aliyekuwa mkuu wataasisi ya Bilal Muslim Mission, anaandika: "Kuswali kwa Kiarabu ni jambo muhimu linaloimarisha uthabiti na umoja wa Waislamu duniani kote. Siku hizi kama Muislamu kutoka Czechoslovakia ataingia msikitini ndani ya Kongo, anajikuta nyumbani na kushiriki katika swala bila ya dalili yoyote ya kuchanganyikiwa. Nini kitatokea ikiwa kila mtu ataambiwa kuswali kwa lugha yake mwenyewe? Je, hisia hii ya umoja inaweza kuishi?"

Hivyo, Uislamu, kama dini ya walimwengu wote, umefungua njia ya kawaida ya kumuelekea Mungu, umewaunganisha wafuasi wake na kuingiza ndani yao hisia ya Udugu wa Milele.

Mtu hawezi kupuuza ubaguzi wa rangi, au utaifa ambao unaenea siku hizi karibu katika kila nchi, Uislamu haujalaani tu kila aina ya ubaguzi lakini umeonyesha njia ya vitendo ya kukuza udugu. Lugha ya pamoja kwa huduma za kidini ina sehemu kubwa katika kuwaleta watu karibu na kila mmoja na kujenga hisia ya usawa machoni pa Mungu.

Qur'an, Kazi ya Mwenyezi Mungu hariri

Lugha ya Kiarabu, ambayo Qur'an na mila za Mtume zimeandikwa kwa lugha hiyo, ina hadhi na heshima maalum kwa mtazamo wa Waislamu. Kwao hadhi hiyo ya juu ya Kiarabu si kwa sababu ni lugha ya Waarabu; badala yake ni kwa sababu ni lugha ya Qur'an iliyochaguliwa na Mwenyezi Mungu kwa kufikisha ujumbe wake wa mwisho na ufunuo wake.

Waislamu wanaamini kwamba Qur'ani Tukufu ni neno la Mungu. Kwa hiyo, inafaa zaidi katika kulisoma neno la Mungu lisomwe kwa lugha ileile ambayo ilisomwa awali. Kiroho, Muislamu mwaminifu anajikuta akizidi kupanda juu kwa msaada wa maneno ya Mungu kama ilivyoelezwa katika lugha ya asili ambayo ni Kiarabu.

Kwa kiasi kikubwa tafsiri haiwezekani hariri

Tafsiri yoyote ya lugha ya asili ya Neno la Mungu haitakuwa neno la Mungu kweli bali kazi ya wanadamu. Ukiendelea kuangalia maarifa yasiyo kamili ya kibinadamu, na kukumbuka kwamba Kiarabu ni lugha pana na tajiri, utalazimika kukubali kwamba hakuna tafsiri ya Qur'an itakayokuwa kamili na ya kutosha kubeba maana ya kweli na kutimiza madhumuni ya kiroho ya kitabu hicho.

Sayyid Sa'eed Akhtar Rizvi anaandika juu ya mada hii: "Kuswali kwa Kiingereza: kwanza kabisa, tafsiri ya kazi yoyote ya fasihi kutoka lugha yoyote kwenda lugha nyingine inachukuliwa na watu wote wa fasihi kama haiwezekani. Bila shaka, utapata maelfu ya tafsiri za kazi za fasihi, lakini zinawakilisha tu mwili wa asili; roho daima hupotea. Pili, lugha ya Kiarabu, hasa, ni ya kina sana kwamba, kwa mfano, haiwezekani tu kufikisha wazo kamili la neno (achilia mbali 'sentensi') kwa Kiingereza. Chukua kwa mfano, maneno ya kawaida ya الحمد لله ambayo kwa ujumla hutafsiriwa kama "Sifa zote ni za Mungu." Sasa ال anawasilisha kwa Kiarabu vivuli vifuatavyo vya maana: 1. Kila kitu kilichotajwa, kuchukuliwa tofauti;

2. Vitu vyote viilivyotajwa kuchukuliwa kwa pamoja;

3. Aina ya kitu kilichotajwa kuchukuliwa kama wazo tofauti n.k Sasa ikiwa unataka kutafsiri ال kwa njia kama vile kufikisha maana zote zilizotajwa hapo juu utalazimika kusema 'Kila mmoja, wote na wote.'

Kisha inakuja حمد . Hakuna neno hata moja kwa Kiingereza la kuwasilisha wazo lake. kama utasema maana yake ni 'Sifa' basi kwa kiarabu itakua ni مدح na si حمد; au ukisema tafsiri yake ni 'Thanks' kwa kiarabu ni شكر na si حمد.

"Hamd" inamaanisha "kumsifu na kumshukuru mtu kwa sababu anastahili kusifiwa kama amekufanyia upendeleo wowote au hakutoa sifa zake ambazo hazijatolewa kwake na mtu mwingine." Mtu yeyote anawezaje kuwasilisha wazo hili katika tafsiri?

Sasa inakuja (L) ya الله inatoa wazo la 'For', 'Ya, 'Mali ya' nk. Hakuna kihusishi kimoja cha Kiingereza kinachoweza kufunika maana zake zote. Kwa ujumla hutolewa kama 'Mungu'. Lakini, kwanza kabisa 'mungu' si tafsiri ya الله kwa sababu الله maana yake ni 'Mtu anayestahili kupendwa' na 'Ambaye kila mtu anatafuta hifadhi kwake.'

Pili الله haina wingi na hakuna jinsia ya kike. Kwa hivyo jina hili lenyewe linaonyesha mwanga juu ya ukweli kwamba Yeye ni mmoja tu na kwamba Hana mshirika wala wa kufananishwa nae. Lakini neno mungu lina wingi (miungu) na kuna mungu wa kike (goddess).

Maelezo haya mafupi yatoshe kuonyesha kwamba haiwezekani kutafsiri Qur'an kwa njia ambayo tafsiri inatoa vivuli vyote vya maana ya asili."

Ni wazi, kwamba hakuna tafsiri inayoweza kuchukua nafasi hii, ya kazi ya fasihi takatifu kabisa. Bila shaka, tafsiri kadhaa za Kiingereza za Qur'an zimechapishwa; lakini daima imehisi kwamba juhudi nyingine ya tafsiri bora inahitajika, kwa sababu tafsiri zote zilizopo zinaonekana kuwa hazitoshi au zinabeba maana za kupotosha za baadhi ya mistari fulani. Hisia hii haizuiliwi kwa tafsiri za Kiingereza tu; Lakini pia huathiri wale walio katika lugha nyinginezo. Katika hali hiyo, je, mtu anapaswa kutumia tafsiri yenye wasiwasi na kuachana na kutumia lugha asili ya fasihi kamili, hasa wakati anahutubia Mwenyezi Mungu?

Tanbihi hariri

  1. Why pray in Arabic? (en). www.al-islam.org (2013-02-03). Iliwekwa mnamo 2022-01-04.