Teinainano (au: South Tarawa) ni mji mkuu wa nchi ya visiwani ya Kiribati katika Pasifiki.

Teinainano (South Tarawa) ni eneo lote kati ya Betio na Bonriki

Manisipaa ya Teinainano (Teinainano Urban Council - TUC) yenye wakazi 36,717 inajumlisha vijiji na miji midogo ya kisiwa kirefu kwenye kusini ya atolli ya Tarawa. Anwani ya kijiografia ni 1°19'N 172°58'E.

Majengo ya serikali yapo hasa mjini Bairiki ambao ni kisiwa kidogo kilichounganishwa na sehemu nyingine za Teinainano kwa madaraja.

Kuna Chuo cha Ualimu cha Kiribati pamoja na tawi la Chuo Kikuu cha Pasifiki ya Kusini. Kuna pia ofisi kuu za makanaisa makubwa.


Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.