The Supremes lilikuwa kundi la waimbaji wa kike kutoka nchini Marekani. Kundi lilikuwa kiungo kikubwa kwa studio ya Motown Records kunako miaka ya 1960.

The Supremes
The Supremes: Diana Ross (kushoto), Mary Wilson (kati), Florence Ballard (kulia) mnamo mwaka wa 1965
The Supremes: Diana Ross (kushoto), Mary Wilson (kati), Florence Ballard (kulia) mnamo mwaka wa 1965
Maelezo ya awali
Pia anajulikana kama The Primettes; Diana Ross & the Supremes
Asili yake Detroit, Michigan,
Marekani
Aina ya muziki Pop, R&B, soul, psychedelic soul, Motown, doo-wop, disco
Miaka ya kazi 1959–1977
Studio Lu Pine (Primettes), Motown (Supremes)
Ame/Wameshirikiana na The Temptations, Four Tops, The Marvelettes
Wanachama wa zamani
Florence Ballard
Diana Ross
Mary Wilson
Betty McGlown
Barbara Martin
Cindy Birdsong
Jean Terrell
Lynda Laurence
Scherrie Payne
Susaye Greene

Awali lilianzishwa likiwa na jina la The Primettes huko mjini Detroit, Michigan, kunako 1959, midundo yao The Supremes ilikuwa pamoja na doo-wop, pop, soul, tuni za maonesho ya Broadway, psychedelic soul, na disco. Lilikuwa kundi lililopata mafanikio makubwa kibiashara kwa Motown, hadi leo, kundi la Kimarekani lililopata mafanikio zaidi[1] likiwa na vibao 12 vilivyoshika nafasi ya kwanza kwenye chati za Billboard Hot 100.

Vibao vikali vingi vilivyotungwa na kutayarishwa na kikosi kikubwa cha utunzi na utayarishaji wa muziki cha Motown, Holland–Dozier–Holland. Wakati wa kilele chao katikati mwa miaka ya 1960, The Supremes walishindana vya kutosha na The Beatles kwa umaarufu dunia nzima,[2] na mafanikio yao yameleta uwezekano wa baadaye kwa wanamuziki wa R&B na soul wa Kiafrika-Kiamerika kupata mafanikio sawa.

Filmografia hariri

Tanbihi hariri

  1. Bronson, Fred: The Billboard Book of Number 1 Hits, page 265. Billboard Books, 2003.
  2. Unterberger, Richie. "The Supremes". Allmusic. Retrieved on 4 Julai 2008.

Marejeo hariri

Soma zaidi hariri

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri