Trakoma (inaitwa pia: vikope, Egyptian ophthalmia[1]) ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na bakteria Klamidia trakomati.[2] Maambukizi husababisha kukwaruza kwa sehemu ya ndani ya vigubiko vya macho. Huo mkwaruzo unaweza kusababisha maumivu ya macho, kuharibika kwa sehemu ya nje ya macho au konea, na hatimaye upofu.[2]

Trakoma
Mwainisho na taarifa za nje
SpecialtyInfectious diseases, ophthalmologist Edit this on Wikidata
ICD-10A71.
ICD-9076
DiseasesDB29100
MedlinePlus001486
eMedicineoph/118
MeSHD014141

Kisababishi hariri

Bakteria inayosababisha ugonjwa unaweza kusambazwa kwa mgusano wa macho au mapua wa moja kwa moja au usiokuwa wa moja kwa moja na mtu aliyeambukizwa.[2] Mgusano wa macho au mapua usiokuwa wa moja kwa moja unajumuisha kupitia nguo au inzi walioguza mtu aliyeambukizwa.[2] Maambukizi mengi huhitajika kwa zaidi ya miaka mingi kabla ya alama iliyoko kwa kigubiko cha jicho haijakuwa kubwa kwamba kope za macho zinaanza kukwaruza jicho.[2] Watoto husambaza ugonjwa kila mara zaidi ya watu wazima.[2] Mazingira chafu, maeneo yaliyo na watu wengi, na pasipo na maji safi ya kutosha na choo yanachangia usambazaji.[2]

Kinga na tiba hariri

Juhudi za kuzuia ugonjwa unajumuisha uboreshaji wa kupata maji safi na kupunguza idadi ya watu walioambukizwa kupitia matibabu ya antibiotiki.[2] Hii inaweza kujumuisha kutibu, wote mara moja, vikundi vyote vya watu vinavyofahamika kuwa na ugonjwa huu kila mara.[3] Kufua nguo haitoshi kuzuia ugonjwa lakini inaweza kuwa bora na hatua zingine.[4] Aina za matibabu hujumuisha azithromycin ya kunywa au tetracycline ya tropikali.[3] Azithromycin hupendelewa kwa sababu inaweza kutumika kama dozi moja tu ya kunywa.[5] Baada ya mkwaruzo wa kigubiko cha jicho kutokea upasuaji unaweza kuhitajika ili kurekebisha sehemu ya kope za macho na kuzuia kuwa kipofu.[2]

Epidemiolojia hariri

Ulimwenguni, takriban watu milioni 80 wako na maambukizi ya hivi karibuni.[6] Katika maeneo mengine maambukizi yanaweza kuwepo kwa ukubwa wa kati ya asilimia 60–90 ya watoto na mara nyingi huathiri wanawake kuliko wanaume kwa sababu ya kuwa karibu na watoto.[2] Ugonjwa huu ni ksababishi cha ukosefu wa kuona vizuri kwa watu milioni 2.2 ambapo milioni 1.2 ni vipofu kabisa.[2] Hutokea mara nyingi kwa nchi 53 za Afrika, Asia, Amerika Kusini na ya Kati na karibu watu milioni 230 wako hatarini.[2] Inachangia hasara ya dola bilioni 8 ya kiuchumi kila mwaka.[2] Ni ya kikundi cha magonjwa kinachojulikana kama magonjwa ya tropikali yasiyozingatiwa.[6]

Marejeo hariri

  1. Swanner, Yann A. Meunier ; with contributions from Michael Hole, TakudzwaShumba&B.J. (2014). Tropical diseases : a practical guide for medical practitioners and students. Oxford: Oxford University Press, USA. p. 199. ISBN 9780199997909. 
  2. 2.00 2.01 2.02 2.03 2.04 2.05 2.06 2.07 2.08 2.09 2.10 2.11 2.12 Blinding Trachoma Fact sheet N°382. World Health Organization (November 2013). Iliwekwa mnamo 14 March 2014.
  3. 3.0 3.1 Evans JR1, Solomon AW (March 2011). "Antibiotics for trachoma". Cochrane Database Syst Rev 16 (3): CD001860. PMID 21412875. doi:10.1002/14651858.CD001860.pub3. 
  4. Ejere, HO; Alhassan, MB; Rabiu, M (Apr 18, 2012). "Face washing promotion for preventing active trachoma.". The Cochrane database of systematic reviews 4: CD003659. PMID 22513915. doi:10.1002/14651858.CD003659.pub3. 
  5. Mariotti SP (November 2004). "New steps toward eliminating blinding trachoma". N. Engl. J. Med. 351 (19): 2004–7. PMID 15525727. doi:10.1056/NEJMe048205. 
  6. 6.0 6.1 Fenwick, A (Mar 2012). "The global burden of neglected tropical diseases.". Public health 126 (3): 233–6. PMID 22325616. doi:10.1016/j.puhe.2011.11.015. 
  Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Trakoma kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.