Udadisi (kwa Kiingereza: "curiosity", kutoka neno la Kilatini "curiositas", yaani "umakini") ni tabia ya kuchunguza kitu au jambo kwa kina[1][2].

Watoto Wazungu wa zamani wakidadisi kamera ya Toni Frissell.

Mara nyingi wanasayansi ndio wadadisi wazuri kwa maana wao huchunguza kwa kina na umakini, wakifuata kanuni na kutafuta ushahidi. Kwa njia yao udadisi umestawisha maisha ya binadamu[3].

Katika udadisi kuna ule wa kawaida na mwingine usio wa kawaida. Kwa udadisi wa kawaida mtu hudadisi kwa njia rahisi, tofauti na ule usio wa kawaida ambapo mtu asipokuwa makini anaweza hata kufa. Udadisi huu unahitaji kuwa makini sana.

Udadisi unajitokeza mapema katika mtoto[4], lakini unapozidi na kuelekea mambo yasiyo na maana (kwa mfano umbeya) unamzuia mtu asijue mambo ya maana; hapo ni kilema cha akili.

Tanbihi hariri

  1. Berlyne DE. (1954). "A theory of human curiosity.". Br J Psychol. 45 (3): 180–91. PMID 13190171. doi:10.1111/j.2044-8295.1954.tb01243.x. 
  2. Berlyne DE. (1955). "The arousal and satiation of perceptual curiosity in the rat.". J Comp Physiol Psychol. 48 (4): 238–46. PMID 13252149. doi:10.1037/h0042968. 
  3. Keller, H., Schneider, K., Henderson, B. (Eds.) (1994). Curiosity and Exploration. New York, N.Y.: Springer Publishing. Kigezo:ISBN missing
  4. Engel, S. 2011. Children’s need to know: Curiosity in schools. Harvard Educational Review. Retrieved from http://www.academia.edu/1268822/Children_s_Need_to_Know_Curiosity_in_Schools

Marejeo hariri