Ufichamishi au kriptografia (kwa Kiingereza: cryptography) ni sayansi ya kulinda mawasiliano kwa kuficha maana yake kwa watu wasiolengwa.

Mashine ya ufichamishi ya Lorenz iliyotumiwa na jeshi la Ujerumani wakati wa Vita Kuu ya Pili.
Mfumo wa kusogeza herufi kwa nafasi 3
Ufichamishaji kwa fimbo

Inajumuisha matumizi ya taratibu za usimbaji (encryption) na kusimbua (decryption) ili kuzuia watu wasiotakiwa au vyombo vya kielektroniki kufikia au kuelewa habari iliyotumwa au kuhifadhiwa. Lengo kuu la cryptography ni kutoa usiri, usalama, na kuthibitisha utambulisho.

Katika muktadha wa teknolojia na usalama wa mtandao, cryptography inatumika sana kuhakikisha usalama wa mawasiliano ya mtandaoni, kama vile barua pepe, manunuzi ya mtandaoni, na mawasiliano mengine ya digitali. Inaweza kutumika pia katika kuhifadhi data ili kuhakikisha kuwa ni salama na haipatikani na watu wasiohitajika.

Kabla ya kupatikana kwa mitambo ya kisasa ujumbe uliandikwa kwa kubadilisha herufi au majina kwa kutumia mfumo uliojulikana kwa mwandishi na mpokeaji aliyelengwa peke yao. Mtu mwingie aliyeona ujumbe alishindwa kuelewa chochote.

Siku hizi ufichamishi hufanywa kwa kutumia mitambo na programu za kompyuta[1].

Cryptography pia ni muhimu katika kuanzisha njia za kuthibitisha utambulisho, ambazo zinahakikisha kuwa watumiaji wanaweza kuaminika na kuthibitishwa kwa usalama katika mazingira ya digital.

Mbinu za ufichamishi sahili hariri

Kati ya mbinu za ufichamishi zilizotumiwa tangu kale ni kubadilishana herufi kufutana na nafasi zao katika alfabeti. Kwa mfano jemadari wa Roma ya Kale, Julius Caesar, alitunga barua za siri akihamisha kila herufi nafasi tatu. Kwa hiyo nafasi ya "a" ilionyesha badala yake herufi "x", "b" ilionyeshwa kwa "y" na kadhalika.

Mfano salamu ya "habari gani" inasomeka hivi kwa kubadilisha nafasi za herufi

  • kusogeza herufi nafasi tatu: "exyxof dakf"
  • kusogeza herufi nafasi tano: "dwxwne cwje"

Mpokeaji anahitaji tu kujua namba ya ufunguo.

Mbinu nyingine ni ufichamishi kwa fimbo lenye kipenyo fulani unaojulikana tangu Ugiriki ya Kale. Kanda ndefu ya ngozi au papiri iliviringishwa kwenye fimbo. Ujumbe uliandikwa mstari kwa mstari. Kanda ilitolewa na kutumwa kwa mpokeaji. Yule alipaswa kuwa na fimbo lenye unene uleule. Akiviringisha kanda mle aliweza kusoma ujumbe. Mtu mwingine aliona tu herufi bila maana. Kama hakuwa na fimbo lenye unene wa kufaa alishindwa kuona herufi katika mistari jinsi zilivyoandikwa.

Marejeo hariri

  • Kahigi, K. K. (2007). Ujanibishaji wa Office 2003 na Windows XP kwa Kiswahili Sanifu. Kioo cha Lugha, 5(1).

Viungo vya Nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  1. Rosenheim, Shawn (1997). The Cryptographic Imagination: Secret Writing from Edgar Poe to the Internet. Johns Hopkins University Press. uk. 20. ISBN 978-0801853319.