Umm al-Quwain (kwa Kiarabu: أمّ القيوين) ni emirati mojawapo ya Shirikisho la Falme za Kiarabu kwenye rasi ya Uarabuni.

Mji wa Umm al-Quwain
Bendera ya Umm al-Quwain.
Falme za Kiarabu.

Iko kaskazini mwa shirikisho, kati ya Ajman na Ras al-Khaimah.

Mtawala wake ni Sheikh Rashid bin Ahmad Al Mu'alla (الشيخ راشد بن احمد المعلا).

Utemi una wakazi 62,000 (2003) katika eneo la km² 750. Haina mapato makubwa kama Abu Dhabi kutokana na mafuta, hivyo imebaki mji mdogo.

Biashara ya wenyeji ilikuwa uvuvi, kujenga maboti ya dhau na kilimo cha mitende katika oasis ya Falaj al-mula. Leo hii utalii umekuwa muhimu.

Viungo vya nje hariri

Magazeti ya Falme za Kiarabu hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Umm al-Quwain kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.