Uroho ni hamu isiyoratibiwa ya kujipatia mali kuliko mtu anavyohitaji, hata kuwakosesha wengine.

Mchoro wa Evelyn De Morgan kuhusu Ibada ya Mamona 1909.
Vilema vikuu

Ni chanzo cha maovu mengi katika maisha ya jamii, kama vile unyonyaji, wizi, vita n.k.

Kwa sababu hiyo maadili ya Kanisa yanauhesabu kati ya vilema vikuu ambavyo vinasababisha dhambi nyingine.

Tena, kadiri ya mtume Paulo, uroho unachangia dhambi zote.