Vicky Ntetema

Mwandishi was habari was BBC


Vicky Ntetema (kuzaliwa c.1958/1959) ni mwandishi wa habari kutoka Tanzania aliyepata umaarufu baada ya kufichua mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini Tanzania. Baadaye akawa mkurugenzi mtendaji wa Under the Same Sun (UTSS) Tanzania.

Vicky Ntetema

Amezaliwa c.1959
Tanzania
Nchi Tanzania
Kazi yake Mwanahabari (BBC), UTSS

Maisha na Kazi hariri

Ntetema alizaliwa nchini Tanzania mwaka 1958. Alipata ufadhili wa kimasomo kutoka serikalini, alisoma nchini Urusi na kupata shahada ya uzamili katika Nyanja ya uandishi habari mwaka 1985. Mnamo mwaka 1991, Ntetema alijiunga na shirika la utangazaji la uingereza BBC kama mtafsiri wa lugha ya kiswahili, baadae akawa mtangazaji katika vipindi vya redio na televisheni jijini London na mwaka 2006 akawa kiongozi wa kitengo na muandishi mkongwe wa BBC World Service nchini Tanzania.[1] Ntetema alijulikana Zaidi mwaka 2007 alipofichua juu ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa Ngozi nchini Tanzania.[2] baadaye Bi. Ntetema aliondoka BBC na akawa mkurugenzi mtendaji wa shirika linaloitwa Under the Same Sun nchini Tanzania, shirika la Canadian linalohamasisha haki za binadamu kwa watu wenye ulemavu wa ngozi. Alijiuzulu mnamo Mei 2018.[3]

Taarifa juu ya kuteswa kwa watu wenye ualbino nchini Tanzania hariri

Uchunguzi mdogo wa Ntetema ulibaini kuwa watanzania wengine waliona watu wenye ualbino kama viumbe wa roho na wachawi wa eneo hilo walizingatia "viungo vyao vya mwili kama viungo vyenye nguvu kwa hirizi za kichawi" huleta mafanikio. [2][4]Taarifa zake zilikuwa na jukumu la kuvutia umakini wa kimataifa kwa hali hiyo. Kwa sababu ya vitisho dhidi yake, Ntetema alilazimika kwenda kujificha, alihitaji kuzunguka saa na alilazimika kuondoka nchini mara mbili kwa usalama wake mwenyewe. .[4][5]

Mnamo mwaka wa 2010, International Women's Media Foundation ilimpa tuzo Courage in Journalism Award kwa taarifa zake. [5][1] In 2016, the U.S. Secretary of State John Kerry awarded Ntetema the International Women of Courage Award.[6][7]

Tuzo hariri

  • Ujasiri katika Tuzo ya Uandishi wa Habari mnamo 2010[5][1]
  • Tuzo ya Wanawake wa Tanzania ya Mafanikio katika jamii "Habari na Mawasiliano" mnamo 2013
  • Tuzo ya kimataifa ya Wanawake wenye Ujasiri mnamo 2016[6][7]

Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 1.2 Wray, Lindsey (2010). "Vicky Ntetema". International Women's Media Foundation. Iliwekwa mnamo 2018-12-11. 
  2. 2.0 2.1 "Tanzania fears over albino killings", BBC News, 2007-12-07. 
  3. Namkwahe, John. "Ntetema announces retirement date from albino lobby group", The Citizen, 2018-04-12. 
  4. 4.0 4.1 Ntetema, Vicky. "In hiding for exposing Tanzania witchdoctors", BBC News, 2008-07-24. 
  5. 5.0 5.1 5.2 "Vicky Ntetema wins bravery award for BBC albino report", BBC News, 2010-05-11. 
  6. 6.0 6.1 "Biographies of 2016 Award Winners Share". U.S. Department of State. Iliwekwa mnamo 2018-12-11. 
  7. 7.0 7.1 "U.S. Embassy Honors 2016 International Women of Courage Laureate Ms. Vicky Ntetema". U.S. Embassy in Tanzania. 2016-12-29. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-06-21. Iliwekwa mnamo 2018-12-12.  More than one of |accessdate= na |access-date= specified (help)
  Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vicky Ntetema kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.