Viktorini wa Camerino

Viktorini wa Camerino (Settempeda, leo San Severino Marche, Italia 470 hivi - Pioraco, 538) alikuwa Mkristo ambaye, alipofiwa wazazi wake, aliamua pamoja na ndugu yake Severino wa Settempeda kuwagawia maskini urithi wao mkubwa na kwenda kuishi upwekeni kwenye Mlima Nero.

Mt. Viktorini akiwa amejitundika mtini kwa toba.

Papa Vigili alimfanya yeye askofu wa Camerino (Italia ya Kati) na Severino askofu wa Settempeda[1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Juni[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. [http://www.santiebeati.it/dettaglio/90942
  2. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.