Wainjili ni waandishi wa vitabu vya Injili vinavyoleta matendo na maneno ya Yesu Kristo.

Simba, mfano wa Mwinjili Marko
Mtu, mfano wa Mwinjili Mathayo

Wakristo wanakubali kama Neno la Mungu vitabu vinne tu vya namna hiyo, yaani vile vilivyoandikwa wakati wa Mitume wa Yesu (karne ya 1 B.K.).

Waandishi wa vitabu hivyo wanatajwa kama Mwinjili Marko, Mwinjili Mathayo, Mwinjili Luka na Mwinjili Yohane.

Ng'ombe, mfano wa Mwinjili Luka
Tai, mfano wa Mwinjili Yohane

Ushuhuda wa kwanza kuwataja pamoja hao wanne ni ule wa Irenei wa Lyons (karne ya 2).

Tangu zamani hao wanne walihusianishwa na viumbehai wanne waliotajwa katika Kitabu cha Ezekieli, halafu katika Kitabu cha Ufunuo: simba, ng'ombe, mtu, tai.

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wainjili kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.