Wamersedari ni watawa wa Shirika la Kifalme, la Kimbingu na la Kijeshi la Bikira Maria wa Huruma na la Ukombozi wa Mateka ambalo lilianzishwa na Petro Nolasco mjini Barcelona, mwaka 1218 ili kukomboa Wakristo waliotekwa na Waislamu kama watumwa. [1][2]

Logo ya shirika.
Basilika la Mercè huko Barcelona lililojengwa lilipokuwepo kanisa mama la shirika mwaka 1267.

Mojawapo kati ya mambo ya pekee ya shirika hilo ni kwamba tangu mwanzo watawa wake wanaweka nadhiri ya nne ya kukubali kufa kwa ajili ya Mkristo aliye katika hatari ya kupoteza imani, kama ilivyokuwa kwa wale waliotekwa utumwani.

Leo shirika linapatikana katika nchi 17.

Tanbihi hariri

  1. Ann Ball, 2003 Encyclopedia of Catholic Devotions and Practices ISBN 087973910X page 525
  2. Mary's Praise on Every Tongue: A Record of Homage Paid to Our Blessed Lady by Chandlery Peter Joseph 2009 ISBN 111316154X page 181

Viungo vya nje hariri