Wilaya ya Kalambo ni wilaya mpya katika mkoa wa Rukwa yenye postikodi namba 55400, ambayo ilianzishwa rasmi mnamo Machi 2012.[1]

Wilaya ya Kalambo
Wilaya ya Kalambo is located in Tanzania
Wilaya ya Kalambo
Wilaya ya Kalambo

Location in Tanzania

Majiranukta: 8°18′12″S 31°31′10″E / 8.30333°S 31.51944°E / -8.30333; 31.51944
Nchi Tanzania
Mikoa Mkoa wa Rukwa

Makao makuu ya wilaya yako Matai.

Mkuu wa wilaya wa kwanza alikuwa Moshi Chang'a. [2]

Wilaya limepokea jina kutoka mto Kalambo unaopita hapa hadi kuishia kweye Maporomoko ya Kalambo upande wa Zambia.

Idadi ya wakazi wa wilaya ilikuwa 207,700 wakati wa sensa ya mwaka 2012. [3] Katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa 316,783 [4].

Uchumi hariri

Eneo la Kalambo liko kati ya Sumbawanga mjini na mpaka wa Zambia. Barabara ni chache na mbaya. Wakazi wengi hulima na kufuga. Mazao ya sokoni ni pamoja na mahindi, alizeti, maharagwa, muhogo na asali.[2] Watu wachache wanalima madini na kuvua samaki.[2]

Utawala hariri

Katika uchaguzi wa bunge la Tanzania Kalambo ni jimbo la uchaguzi.[5]

Kata hariri

Wilaya ya Kalambo huwa na kata 17:[6]

  • Kalambazite
  • Kasanga
  • Katazi
  • Katete
  • Kisumba
  • Legeza Mwendo
  • Mambwe Kenya
  • Mambwe Nkoswe
  • Matai

  • Mkali
  • Mkowe
  • Mnamba
  • Msanzi
  • Mwazye
  • Mwimbi
  • Sopa
  • Ulumi

Marejeo hariri

  1. Staff. "Tanzania: State Gazettes New Regions, Districts", 9 March 2012. Retrieved on 2014-01-13. Archived from the original on 2012-08-23. 
  2. 2.0 2.1 2.2 Siyame, Peti. "Tanzania: Truance Irks Kalambo DC", 3 July 2012. 
  3. Sensa ya 2012, Rukwa - Kalambo District Council
  4. https://www.nbs.go.tz
  5. Organisations located in Rukwa Region - Tanzania. African Development Information. Jalada kutoka ya awali juu ya 2018-06-01. Iliwekwa mnamo 2014-01-13.
  6. Postcodes Rukwa Region 55000. Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) (2012). Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-08-31. Iliwekwa mnamo 2014-01-13.
  Kata za Wilaya ya Kalambo - Mkoa wa Rukwa - Tanzania  

Kanyezi | Kasanga | Katazi | Katete | Kilesha | Kisumba | Legezamwendo | Lyowa | Mambwekenya | Mambwe Nkoswe | Matai | Mbuluma | Mkali | Mkowe | Mnamba | Mpombwe | Msanzi | Mwazye | Mwimbi | Samazi | Sopa | Sundu | Ulumi

  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Rukwa bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Kalambo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.