Wilaya ya Tarime ni wilaya mojawapo kati ya 9 za Mkoa wa Mara. Zamani ilijulikana kwa jina la "Wilaya ya Mara Kaskazini". Mwaka 2006 sehemu ya mashariki ya Tarime imekuwa wilaya mpya ya Rorya.

Mahali pa Tarime (kijani cheusi) katika Mkoa wa Mara (kijani) na Tanzania kwa jumla.


Tarime
Wilaya ya Tarime
Mahali pa Wilaya ya Tarime
Mahali pa Wilaya ya Tarime
Mahali pa Wilaya ya Tarime
Tarime is located in Tanzania
Tarime
Tarime

Mahali pa Wilaya ya Tarime

Majiranukta: 1°24′51″S 34°27′51″E / 1.4141°S 34.4642°E / -1.4141; 34.4642
Nchi Tanzania
Mkoa Mkoa wa Mara
Wilaya Tarime
Eneo
 - Jumla 1,371 km²
Idadi ya wakazi (Sensa ya 2022)
 - Wakazi kwa ujumla 404,848
EAT (UTC+3)
Tovuti:  https://tarimedc.go.tz

Tarime imepakana na Kenya (kaunti za Migori, Trans Mara na Kisii) upande wa kaskazini na mashariki. Hifadhi ya wanyama ya Masai Mara ya Kenya uko upande wa mashariki pia. Upande wa kusini umepakana na wilaya za Musoma mjini, Musoma vijijini na wilaya ya Serengeti. Upande wa magharibi iko wilaya mpya ya Rorya.

Makao makuu ya wilaya yapo mjini Tarime.

Misimbo ya posta katika wilaya hii inaanza kwa 314.

Wakazi hariri

Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 339,693[1] na katika ile ya mwaka 2022, baada ya kumegwa, walihesabiwa 404,848 [2].

Tarime ni eneo la Wakuria hasa, waliopo pia ng'ambo ya mpaka nchini Kenya. Wakazi asilia wengine ni Wasimbiti.

Wakazi wengi ni wakulima na wafugaji wa wanyama kama vile ng'ombe, mbuzi na kondoo. Eneo la Tarime linajulikana kwa matatizo ya mapigano ya mara kwa mara kati ya wakulima na wafugaji.

Migodi ya dhahabu hariri

Karibu na kijiji cha Nyamongo katika kata ya Nyamwaga kuna migodi ya dhahabu ya North Mara Gold Mine inayomilikiwa na kampuni Acacia Mining kutoka Uingereza. Kuwepo kandokando kwa utajiri wa dhahabu na umaskini wa wenyeji kunasababisha mara kwa mara kuingia kwa wanavijiji katika eneo la migodi wanapojaribu kukusanya mtapo wenye dhahabu.

Mwaka 2011 na 2013 wanavijiji kadhaa walioingia katika eneo la migodi waliuawa na maafisa wa polisi waliosaidia walinzi wa kampuni[3][4]. Mashirika ya haki za binadamu yalishtaki kampuni kwa niaba ya wahanga mbele ya mahakama huko Uingereza. Kesi zilisimamishwa mwezi wa Fevruari 2015 baada ya kampuni kulipa fidia kwa familia husika.[5][6]

Marejeo hariri

  1. Sensa ya 2012, Mara - Tarime-District-Council
  2. https://www.nbs.go.tz
  3. http://www.bloomberg.com/news/articles/2010-12-23/shooting-gold-diggers-at-african-mine-seen-amid-record-prices Shooting Gold Diggers at African Mine Seen Amid Record Prices, Bloomberg.com December 23, 2010
  4. http://www.facing-finance.org/en/database/cases/violence-at-north-mara-goldminegewalt-und-vertreibung-bei-der-goldmine-in-north-mara/ Archived 1 Novemba 2015 at the Wayback Machine. Barrick Gold: Human Rights Violations in Tanzania, Facing Finance database
  5. http://business-humanrights.org/en/african-barrick-gold-lawsuit-re-tanzania African Barrick Gold lawsuit (re Tanzania) Business & Human Rights Resource Center
  6. http://www.theguardian.com/environment/2015/feb/10/british-gold-mining-settlement-deaths-tanzanian-villagers British gold mining firm agrees settlement over deaths of Tanzanian villagers Guardian newspaper (UK) Tuesday 10 February 2015

Viungo vya Nje hariri

  Kata za Wilaya ya Tarime Vijijini - Mkoa wa Mara - Tanzania
 

Binagi * Bumera * Ganyange * Gorong'a * Gwitiryo * Itiryo * Kemambo * Kibasuka * Kiore * Komaswa * Kwihancha * Manga * Matongo * Mbogi * Muriba * Mwema * Nyakonga * Nyamwaga * Nyansincha * Nyanungu * Nyarero * Nyarokoba * Pemba * Regicheri * Sirari * Susuni


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mara bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Tarime kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Usiingize majina ya viongozi au maafisa wa sasa maana wanabadilika haraka mno.