Yese au Yishai (kwa Kiebrania: יִשַׁי, Yišay, Yīšáy, maana yake "Mfalme" au "Mungu yupo" au "Zawadi ya Mungu"; kwa Kigiriki: Ἰεσσαί, Iessai; kwa Kilatini: Isai, Jesse) ni mtu anayetajwa na Biblia kama baba wa mfalme Daudi wa Israeli. Huyu pengine anatajwa tu kama "Mwana wa Yese" (Ben Yishai). Hivyo anatajwa pia katika orodha ya vizazi vya Yesu (Math 1:1-17).

Yesse katika kioo cha rangi, All Saints Church, Hove, Sussex, Uingereza.

Baba yake alikuwa Obedi, mwana wa Boazi na Ruthu. Kama hao wote aliishi Bethlehemu.

Mtu wa kabila la Yuda, alizaa watoto saba wa kiume, Daudi akiwa wa mwisho wao.[1] Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati kinawataja hivi: Eliabu, Abinadabu, Shimea, Nethaneli, Raddai, Ozem na Daudi mbali ya mabinti wawili, Zeruia and Abigaili.[2]

Tanbihi hariri

  1. 1 Sam 16:6-16:11
  2. 1 Nya 2:13-16

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yese kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.