Zakayo (kwa Kigiriki Ζακχαῖος, Zakkhaios; kwa Kiebrania זכי, "safi", "asiye na kosa"[1]) alikuwa mtozaushuru tajiri mjini Yeriko aliyepata umaarufu kupitia Injili ya Luka ambayo katika sura ya 19 inasimulia alivyoongoka alipomkaribisha Yesu Kristo nyumbani mwake kwa kumuahidia atawagawia mafukara nusu ya mali yake na kuwarudishia mara nne watu aliowadhulumu kitu.

Painting showing Jesus holds up his hand to call Zacchaeus down from the tree while a crowd watches
Zakayo alivyochorwa na Niels Larsen Stevns. Yesu anamuita Zakayo ashuke toka juu mtini.
Photo of the actual Sycamore fig tree in Jericho today.
Mkuyu wa huko Yeriko leo.
Stained glass rendition of Zacchaeus receiving Jesus into his house.
"Zakayo akimlaki Yesu",
Kanisa la Mchungaji Mwema, Yeriko.

Kwa kumtafuta mtu kama huyo, aliyetazamwa na Wayahudi kama mpotevu kutokana na kazi yake haramu kwao, Yesu alidhihirisha kwamba alikuja kutafuta waliopotea, wakiwemo matajiri wanaokubali kuachana na uroho ili kujali shida za wengine. Hiyo ni mada muhimu katika Injili hiyo.

Zakayo ni mfano wa kuigwa na matajiri wa leo. Matajiri kwa kawaida yao ni watu wanaojali faida kwa gharama yoyote ile, kwa kupokonya cha maskini ili wafaidike wao. Wanajihalalishia kuwa ni haki yao kuwa matajiri na kuwasahau maskini. Wanachojali ni pesa iingie mifukoni mwao na si vinginevyo.

Inasemekana baadaye alikuwa askofu wa kwanza wa Kaisarea ya Palestina[2]..

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 20 Agosti au 27 Agosti au 20 Aprili au tarehe nyingine[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Milligan, Jim. Lexicon :: Strong's G2195 - Zakchaios. Blue Letter Bible. Sowing Circle.
  2. http://www.ccel.org/ccel/schaff/anf07.ix.viii.iv.html
  3. http://www.santiebeati.it/dettaglio/93257

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Zakayo kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.