Masimo na Domasi (walifariki 380) walikuwa watoto wa gavana Valentiniani aliyewalea Kikristo[1].

Baada ya kwenda Nisea (leo nchini Uturuki)[2][3] walihamia Siria kama wamonaki na hatimaye jangwani Misri karibu na Makari Mkuu[4][5][6][7].

Walikuwa wa kwanza kufariki huko Skete[5] na Makari alijenga kanisa la kwanza huko jangwani pale walipokuwa wanaishi.

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakopti kama watakatifu[8][5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Januari.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.