Mesrop Mashtots (pia Mesrob Mashtotz, kwa Kiarmenia Մեսրոպ Մաշտոց; Hatsik, Armenia ya Kale, leo nchini Uturuki, 361 hivi - Wagharshapat, Armenia, 17 Februari 440) alikuwa mmonaki, mwanateolojia, mshairi na mtaalamu wa lugha mwanafunzi wa Patriarki Nerses I.

Mesrop Mashtots alivyochorwa mwaka 1776.
Mesrop Mashtots alivyochorwa na Francesco Maggiotto (1750-1805).
Monasteri ya Amaras huko Nagorno Karabakh ambapo Mesrop Mashtots alianzisha shule ya kwanza iliyotumia alfabeti yake.[1]

Anaitwa "Mwalimu wa Armenia" kwa kuwa ndiye aliyebuni alfabeti ya Kiarmenia (406) ili waamini waweze kujua Biblia ya Kikristo akaitafsiri yote akaanzisha shule nyingi akiweka hivyo misingi ya taifa hilo na ustaarabu wake uliolidumisha hata leo kati ya matatizo makubwa ya historia yake, hasa dhuluma za kidini.

Baada ya kufanya kazi ikulu, alipata daraja takatifu na kujiunga na umonaki akaanzisha mtindo wa monasteri kuwa na shule karibu nayo ili kuandaa watu watakaoendeleza elimu ya dini hasa kwa kutafsiri na kunakili vitabu.

Mapema monasteri kubwa zikawa pia na seminari kuu au vyuo vikuu vya teolojia.

Hivyo umonaki wa Armenia ulidumisha utamaduni wa taifa hilo, ambalo lilikuwa la kwanza kupokea Ukristo jumla pamoja na mfalme wake (300) halafu likaushika moja kwa moja hata lilipopitia vipindi vigumu sana.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Viviano, Frank. “The Rebirth of Armenia,” National Geographic Magazine, March 2004
  2. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

Filamu hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.