Nchi huru ni zile ambazo hazitawaliwi na nchi nyingine. Kauli hiyo haimanishi kwamba wananchi wake ni huru, kwa sababu pengine mfalme au rais ni mwenyeji, lakini anawanyima haki zao kwa kiasi hata kikubwa (ambacho kinaitwa udikteta).

Makoloni kumi na tatu ya Uingereza katika Amerika Kaskazini yakitoa tamko la kujitangaza huru mwaka 1776.
Chile, koloni mojawapo la Hispania katika Amerika Kusini, ilifanya vilevile mwaka 1818.

Mara nyingi nchi inajitangaza huru, halafu inatambuliwa na nchi nyingine kuwa hivi. Kama si nchi zote zinatambua rasmi uhuru wake, hali ya kisheria inabaki tata.

Siku hizi duniani kuna nchi huru karibu 200, ya mwisho kutambulika ikiwa Sudan Kusini (2011) na ndogo zaidi ikiwa Mji wa Vatikano (km2 0.44 na wakazi 600 hivi tu).

Hii haiuzii nchi kuingiliwa kwa namna moja au nyingine kama vile katika ukoloni mamboleo.