Paul Rusesabagina (alizaliwa Murama, Gitarama, Rwanda, 15 Juni 1954) ni raia wa Rwanda aliyekuwa meneja wa Hotel des Mille Collines mjini Kigali. Wakati wa mauaji ya kimbari ya Rwanda aliwalinda Wahutu na Watutsi waliokimbilia hoteli yake na hivyo kuokoa watu 1268 dhidi ya wanamgambo wa Interahamwe.

Rusesabagina, 2006

Kazi wa Paul Rusesabagina ilikuwa msingi wa filamu ya “Hotel Rwanda” iliyofanyika mwaka 2004. Rusesabagina alionyeshwa na Don Cheadle, mwigizaji wa Marekani.

Anaishi katika mji wa Brussels katika nchi ya Ubelgiji na mji wa San Antonio katika jimbo la Texas nchi ya Marekani. Yeye ana nyumba katika miji miwili.

Rusesabagina alianza “Hotel Rwanda Rusesabagina Foundation” kupigania haki za binadamu duniani.[1]

Kuzaliwa na Kazi hariri

Paul Rusesabagina alizaliwa katika mji wa Murama katika nchi ya Rwanda. Rusesabagina alikuwa na kaka na dada nane: baba yake alikuwa Mhutu na mama yake alikuwa Mtutsi. Rusesabagina alikwenda shule katika mji wa Gitwe na wakati alipokuwa na miaka 13, aliweza kuzungumza kwa Kiingereza na Kifaransa. Alioa mke wake wa kwanza mwaka 1967. Mwisho wa ujana wake, alitaka kuwa mchungaji. Hivyo, yeye na mke wake walihamia Kamerun aliposoma katika chuo cha theolojia.

Mwaka 1978, yeye, mke wake, na watoto wake walirudi mji wa Kigali. Rusesabagina alipewa nafasi katika Hotel des Mille Collines akatumwa Uswisi na Brussels kusoma uongozi wa hoteli. Yeye na mke wake wa kwanza walitengana kwa sababu ya umbali. Miaka sita baadaye alikutana na Tatiana aliyekuwa muuguzi katika mji wa Ruhengeri. Paul alimuoa Tatiana miaka miwili baadaye. Tatiana alichukua watoto wa Paul na Paul na Tatiana baadaye walikuwa na mtoto pamoja, aliitwa Tresor.

Mwaka 1992 Rusesabagina alipandishwa cheo kuwa meneja mkuu katika “Diplomates Hotel”, mshirikia wa Hotel des Mille Collines.

Mauaji ya Kimbari hariri

Katika nchi ya Rwanda, wakati Paul alipopokea elimu huko Nairobi, Uswisi na Brussels, serikali ya Rais Juvénal Habyarimana ilikabiliwa na mashambulizi ya wanamgambo ya NRA chini ya Yoweri Museveni kwenye maeneo ya mpaka na Uganda. Kundi la NRA iliunganisha wakimbizi Watutsi pale Uganda na Wahutu wapinzani wa serikali. Uvumi ulioletwa na kituo cha redio RTLM ulisambazwa kuwa Watutsi walitaka kuua Wahutu wote.

Tarehe 6 Aprili 1994, ndege ya Habyarimana ilipigwa na roketi kabla ya kutua kwenye uwanja wa ndege wa Kigali. Mara moja wanajeshi pamoja na viongozi wa Interharamwe waliamuru kuwaua Watutsi wote nchini pamoja na wapinzani wengine. Wakati vurugu ilipoanza, Rusesabagina alileta familia yake kwenye Hôtel des Mille Collines kwa usalama. Wakimbizi walijunga nao katika hoteli.[2]

Rusesabagina alifaulu kuzuia wanamgambo wa Interharamwe kuingia katika hoteli na kuua wageni wake hadi kufika kwa jeshi la NRA lililofukuza wanamgambo na mabaki ya serikali ya Habyarimana.

Rusesabagina pamoja na familia yake walikimbilia Tanzania na kutoka huko baadaye hadi Ubelgiji. Aliendelea kutishiwa hata ng'ambo, hivyo alihamia tena Marekani anapoishi.

Mnamo Septemba 2021, Paul Rusesabagina alihukumiwa kwa ugaidi, mwendesha mashtaka aliomba dhidi yake maisha yote.

Tanbihi hariri

  1. "'Hotel Rwanda' Manager: We've Failed To Learn From History". National Public Radio. April 5, 2014. Retrieved February 21, 2015.
  2. Melvern, Linda (2006). Conspiracy to Murder: The Rwandan Genocide. Verso.
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Paul Rusesabagina kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.