Kwintiani wa Rodez

(Elekezwa kutoka Quintiani wa Rodez)

Kwintiani (kwa Kilatini: Quintianus, Quinctianus; kwa Kifaransa: Quintien; alifariki 13 Novemba 525 au 526) alikuwa askofu wa Rodez, halafu wa Clermont-Ferrand (Arvernes) katika karne ya 6, na kwa msingi huo alishiriki Mtaguso wa Agde (508) na Mtaguso wa kwanza wa Orléans (511).

Kwintiani katika kioo cha rangi.

Kadiri ya Gregori wa Tours alizaliwa barani Afrika. Akiwa padri wa Karthago alikimbilia Ufaransa kutokana na dhuluma za Wavandali dhidi ya Wakatoliki[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2], lakini pia 14 Juni[3][4].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.