Roboti ya viwandani

Roboti ya viwandani (kwa Kiingereza: industrial robot) ni mfumo wa roboti unaotumika katika uzalishaji wa bidhaa. Roboti za viwandani ni za kiotomatiki, zinaweza kupangwa na zinaweza kusonga kwa ekseli tatu au zaidi.

Seti ya roboti za ekseli sita zinazotumika kuchomelea.

Roboti za viwandani hutumiwa kwa shughuli kama kuchomelea vyuma, kupaka rangi, kuunganisha na kutenganisha, [1] kuchukua na kuweka vipuli kwa bodi za saketi zilizochapishwa, kuweka lebo, ukaguzi wa bidhaa na majaribio; yote yametimizwa kwa kasi, na usahihi. Zinaweza kusaidia katika utunzaji wa nyenzo.

Katika mwaka wa 2020, roboti za viwandani milioni 1.64 zilikuwa zikifanya kazi kote ulimwenguni kulingana na Shirikisho la Kimataifa la Roboti (IFR). [2]

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Roboti ya viwandani kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.