Sofroni wa Yerusalemu

Sofroni wa Yerusalemu (Damasko, Syria[1], 560 hivi - Yerusalemu, Israeli/Palestina, 11 Machi 638) alikuwa askofu wa Yerusalemu kuanzia mwaka 634 hadi kifo chake[2][3]. Wakati huo Yerusalemu ulitekwa na Waarabu Waislamu naye alitetea imani na haki za wananchi dhidi ya wavamizi.

Mt. Sofroni alivyochorwa.

Kabla ya hapo alikuwa mwanafunzi wa Yohane Mosko akaongozana naye kutembelea monasteri nyingi, akawa mwalimu, halafu mmonaki mwanateolojia aliyetetea vizuri imani sahihi kuhusu Yesu Kristo kuwa na utashi wa kibinadamu chini ya ule wa Kimungu.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 11 Machi[4].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. "St. Sophronius the Patriarch of Jerusalem", Orthodox Church in America
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/90499
  3. John F. Matthews, "Sophronius, ‘the Sophist’," in Simon Hornblower, Antony Spawforth and Esther Eidinow (eds.), The Oxford Classical Dictionary, 4th ed. (Oxford University Press, 2012). ISBN 9780191735257
  4. Martyrologium Romanum, 2004

Marejeo hariri

  • D. Woods, 'The 60 Martyrs of Gaza and the Martyrdom of Bishop Sophronius of Jerusalem’, ARAM Periodical 15 (2003), 129–50. Reprinted in M. Bonner (ed.), Arab-Byzantine Relations in Early Islamic Times (Aldershot, 2005), 429–50.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.