Sumo (相撲, sumō) ni michezo ya miereka kutoka nchini Japani.[1]

Mechi ya Sumo.

Katika Sumo ni wapiganaji wawili (wanaitwa rikishi) wanaoshindana wakiangaliwa na refa. Mashindano hutekelezwa katika mviringo wenye kipenyo cha mita 4.55.

Kila mpiganaji analenga ama kumsukuma mwenzake nje ya mviringo, au kumlazimisha kugusa sakafu na sehemu yoyote ya mwili wake isipokuwa nyayo.

Kila mwaka kuna mashindano (basho) makubwa yanayotekelezwa katika miji hufanyika Tokyo, Osaka, Nagoya na Fukuoka. Idadi ni mashindano 6 makuu ya kitaalamu (inayojulikana kama honbasho) kwa mwaka, kwenye miezi ya Januari, Machi, Mei, Julai, Septemba na Novemba.

Mashindano kawaida hudumu kwa siku 15 na huonyesha mechi kutoka kwa migawanyiko tofauti. Nafasi 5 za juu zinajulikana kama "Mgawanyiko wa Juu", pia huitwa Makuuchi (幕 内) au Makunouchi (幕 の 内). Kila shindano huwa na rikishi 42.

Mabingwa wakuu hariri

Wale ambao wamepata kiwango cha juu zaidi ni mabingwa wakuu (yokuzuna). [2]

  • Akashi, karne ya 16 [2]
  • Maruyama, (1712-1749)
  • Tanikaze (Kajinosuke, 1750-1795)
  • Onagawa (1758-1805)
  • Ao no Matsu (1791-1851)
  • Chiyonofuji Mitsugu (b. 1955) [3]
  • Takanosato (b. 1952) [2]
  • Futahaguro Koji (b. 1963)
  • Hokuto-umi, (b. 1963)
  • Onokuni (b. 1962)
  • Asahifuji (b. 1960)
  • Akebono (b. 1970)

Marejeo hariri

  1. Nussbaum, Louis-Frédéric. (2005). "Sumo" in Japan Encyclopedia, p. 914.
  2. 2.0 2.1 2.2 Nussbaum, "Yokozuna (Sumo Grand Champions)" at p. 915; retrieved 2012-2-27.
  3. Nussbaum, "Chiyonofugi" at p. 117; retrieved 2012-2-27.
  Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu zaidi kuhusu Sumo kama historia yake, uenezi au kanuni zake?
Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.