Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 1972

Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 1972 ulikuwa wa 47 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 7 Novemba. Upande wa "Republican Party", Rais Richard Nixon (pamoja na kaimu wake Spiro Agnew) alimshinda mgombea wa "Democratic Party" George McGovern (pamoja na kaimu wake Sargent Shriver).

Matokeo hariri

Nixon akapata kura 520, na McGovern 17 wakati mchaguzi mmoja kutoka Virginia alimpigia kura John Hospers badala ya Nixon. Ramani yaonyesha kura kwa kila jimbo.