Urujuani
Urujuani ni rangi kati ya buluu na nyekundu. Iko karibu na zambarau lakini inaelekea zaidi upande wa buluu.
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/76/Color_icon_violet_v2.svg/220px-Color_icon_violet_v2.svg.png)
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/17/Color_icon_purple.svg/220px-Color_icon_purple.svg.png)
Ni rangi ya saba ya upinde wa mvua. Kifizikia ni rangi ambayo mawimbi yake ni fupi zaidi kati ya rangi zinazoonekana kwa binadamu; kama ni fupi zaidi inaendelea kuwa urujuanimno ambayo haionekani kwa macho yetu.