Amalek

(Elekezwa kutoka Waamaleki)

Amalek (kwa Kiebrania עֲמָלֵק, ʻĂmālēq [1]) ni jina linalopatikana katika Biblia ya Kiebrania, kwa hiyo pia katika Agano la Kale la Biblia ya Kikristo, kuhusu mjukuu mmojawapo wa Esau, kabila la wahamaji lililotokana naye (Waamaleki), na maeneo yaliyokaliwa nao[2] (Negev, Moabu na jangwa la Sinai) ambayo katika karne ya 14 KK yalikuwa na wakazi wachache sana.

Mchoro wa Gustave Doré, Kifo cha Agag. Inawezekana "Agag" lilikuwa jina la kurithiwa la wafalme wote wa Amalek. Aliyechorwa aliuawa na Samweli (1 Sam 15).

Waisraeli walipohama Misri, Waamaleki walikuwa wa kwanza kupigana nao[3] wakawa maadui wao wa kudumu mpaka walipoangamizwa na mfalme Sauli.

Tanbihi hariri

  1. Amalek may mean people of lek (עֲם , לֵק), or "dweller in the valley", or possibly "war-like", "people of prey", "cave-men". Z'ev ben Shimon Halevi, Kabbalah and Exodus,Weiser Books 1988 p.101.
  2. J. Macpherson, 'Amalek' in James Hastings, (ed.) A Dictionary of the Bible: Volume I (Part I: A -- Cyrus), Volume 1, University Press of the Pacific, Honolulu, (1898) 2004, pp.77-79,p.77.
  3. Rashi [1]

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Amalek kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.