Zuchu
'
Zuhura Othman Soud | |
---|---|
Amezaliwa | 12 Oktoba 1993 |
Majina mengine | Zuchu |
Kazi yake | Msanii |
Zuhura Othman Soud (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii Zuchu; alizaliwa 22 Novemba 1993[1]) ni mwanamuziki, mtunzi wa nyimbo na msanii wa kurekodi wa Kitanzania aliezaliwa Zanzibar. Amesainiwa chini ya lebo ya WCB Wasafi Records chini ya uongozi wa Diamond Platnumz. [2] [3][4]
Alitunukiwa tuzo ya silver play button na mtandao wa kijamii wa Youtube kwa kuwa msanii wa kwanza wa kike Afrika mashariki kwa kufikisha wafuasi zaidi ya 100,000 ndani ya wiki moja.[5]
Katika wiki ya kusheherekea siku yake ya kuzaliwa, Zuchu alitunukiwa tuzo ya msanii bora chipukizi wa mwaka 2020 na All Africa Music Awards|AFRIMMA.[6]
Maisha ya awali hariri
Zuchu amezaliwa kwenye familia ya wanamuziki . Ni binti wa mwanamuziki wa taarabu anayefahamika kwa jina la Khadija Kopa.[7][8][9][10] Zuchu alianza kuimba akiwa na umri mdogo na baadae kushirikiana na mama yake Khadija Kopa katika wimbo unaofahamika kama Mauzauza [11]
Zuchu alitambulika rasmi kwenye Tasnia ya muziki mnamo Aprili 2020. [12] Mpaka sasa ana albamu moja na alichaguliwa kushiriki mashindano ya kuwania tuzo ya MTV, MAMA awards ya mwaka 2021. Kwenye mashindano hayo, Zuchu amepangwa katika kipengele cha 'best breakthrough act', anakabiliwa na ushindani kutoka kwa Elaine na Focalistic wa Afrika Kusini na Tems na Omah Lay wote kutoka Nigeria, John Blaq (Uganda) na Sha Sha (Zimbabwe). Mpaka sasa ana albamu moja na alichaguliwa kushiriki mashindano ya kuwania tuzo ya MTV, MAMA awards ya mwaka 2021. Kwenye mashindano hayo, Zuchu amepangwa katika kipengele cha 'best breakthrough act', anakabiliwa na ushindani kutoka kwa Elaine na Focalistic wa Afrika Kusini na Tems na Omah Lay wote kutoka Nigeria, John Blaq (Uganda) na Sha Sha (Zimbabwe).[13]
Albamu hariri
Zuchu aliachia albamu ya kwanza iliyotambulika kama “ I am Zuchu “ mwaka 2020 ikiwa na nyimbo 7. [14] Albamu yake ndiyo iliyosikilizwa na watu wengi zaidi nchini Tanzania kwa mwaka 2020 na vidio za nyimbo zake zimetazamwa na mamilioni ya watu.[15]
Nyimbo zake hariri
Mwaka | Nyimbo | Albamu |
---|---|---|
2020 |
"Hakuna Kulala" | I Am Zuchu EP |
"Nisamehe" | ||
"Kwaru" | ||
"Wana" | ||
"Raha" | ||
"Ashua"(feat. Mbosso) | ||
"Tanzania ya Sasa" | ||
"Shangilia" | ||
"Mauzauza"(feat. Khadija Kopa) | ||
"Cheche" (feat. Diamond Platnumz) | ||
"Litawachoma" (feat. Diamond Platnumz) | ||
"Hasara" | ||
"Nobody" (feat. Joeboy) | ||
2021 |
"Sukari" |
Marejeo hariri
- ↑ Zuchu – YouTube.
- ↑ Zuchu Bio – Age, Career, Education, Songs, WCB, Boyfriend, Net Worth (en).
- ↑ Zuchu is the new face on Diamond's record label WCB.
- ↑ Zuchu set to rise under the auspices of Diamond Platnumz (en) (17 July 2020).
- ↑ Zuchu set to rise under the auspices of Diamond Platnumz (en) (17 July 2020).
- ↑ Check out full list of winners at the 2020 AFRIMMA Awards (en-US) (16 November 2020).
- ↑ Diamond's new signee Zuchu features her mum, legendary Khadija Kopa, in new song days after joining WCB.
- ↑ Kati ya wasanii hawa mmoja atajiunga WCB.
- ↑ Diamond's new signee Zuchu features her mum, legendary Khadija Kopa, in new song days after joining WCB.
- ↑ Kati ya wasanii hawa mmoja atajiunga WCB.
- ↑ ZUCHU – Biography – Age, Family, Early life, Record Label, Music, Net Worth. Jalada kutoka ya awali juu ya 2021-03-04. Iliwekwa mnamo 2021-03-06.
- ↑ Why WCB’s new signee Zuchu is a force to reckon with as she unveils her EP ‘I am Zuchu’.
- ↑ Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2021-02-25. Iliwekwa mnamo 2021-03-06.
- ↑ Zuchu: I Am Zuchu.
- ↑ https://www.thecitizen.co.tz/tanzania/news/entertainment/zuchu-named-on-bbc-s-10-african-musicians-to-look-out-for-in-2021-3245486
Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Zuchu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |