Mtumiaji:Zenman/Mradi wa Afrika

Makala iliyochaguliwa hariri

Makala iliyochaguliwa kwa Mei 2012 hariri

 
Eneo la Zanj ya kihistoria kwenye ramani ya Afrika ya Mashariki

Zanj (Kiarabu na Kifarsi زنج) ni neno lililotumiwa na waandishi Waislamu wa zamani kutaja watu weusi kutoka Afrika ya Mashariki na pia kwa maana ya kijiografia kutaja eneo la Afrika ya Mashariki. Wanajiografia Waislamu walihesabu pwani takriban kati ya Mogadishu na kisiwa cha Pemba kuwa "Zanj". Kusini yake waliita nchji ya Sofala na kaskazini yake nchi ya Berbera kufuatana na mabandari ya nyakati ziule zilizojulikana kwao. Uwezekano mkubwa ni neno hili Zanj latokana na jina la kijiografia la awali "Azania" likatumiwa baadaye kutaja hasa kisiwa cha Zanzibar. Baadaye Zanj imejulikana kama nchi ya Waswahili. Waandishi Waarabu wa kale waliita hasa watu weusi kutoka Afrika ya Mashariki kwa jina hili la "Zanj". Waliwatofautiana na Waafrika weusi wengine kama Wanubia (taz. Nubia) au Wahabash (taz. Uhabeshi). Walitazamiwa kuwa watu wenye hali na maendeleo ya duni kulingana na wenyeji wengine wa Afrika iliyojulikana kwa Waarabu.


Je, wajua...? hariri


Wasifu Uliochaguliwa hariri

Wasifu Uliochaguliwa kwa Mei 2012 hariri

 
Picha ya Shaka Zulu mnamo mwaka 1824

Shaka (pia: Tshaka, Tchaka au Chaka; halafu: Shaka Zulu, Shaka ka Senzangakhona) (* takriban 1781 - 1828 BK) alikuwa kiongozi wa Wazulu aliyebadilisha ukoo mdogo wa Kinguni kuwa kabila au taifa kubwa lililotawala maeneo mapana ya Afrika Kusini hasa Natal ya leo. Sifa zake zimetokana na uwezo wa kupanusha utawala wake kutoka eneo ndogo la 260 km² kuwa 28.500 km², kuvunja nguvu ya makabila mengine na kuyaunganisha na taifa lake. Katika historia ya kijeshi ya Afrika alianzisha mbinu mpya zilizopanusha uwezo na enzi yake.


kuchaguliwa picha kwa 2012 hariri

kuchaguliwa picha kwa Mei 2012 hariri

 


Murchison Falls kutoka juu, Uganda
(kupata bango)